Kuwa Na Moyo Wa Kusamehe

Waa’il bin Hujr (Radhiyallahu anhu) alikuwa sahaabi maarufu wa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) ambaye alitoka katika nchi ya Yemen na kutoka katika kizazi cha wafalme.

Inaripotiwa kwamba wakati aliondoka Yemen kuja Madinah Munawwarah kusilimu, basi kabla ya kusiliku, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) aliwajulisha maswahaabah kama amefika.

Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) aliwaambia maswahaabah (Radhiyallahu anhum), “Kuna mtu ambaye anakaribia kufikia Madinah Munawwarah kutoka nchi ya Hadramowt huko Yemen. Anakuja na nia ya Kusilimu, na anatoka katika kizazi cha wafalme. Jina lake ni Waa’il bin Hujr. ”

Alipofika, Rasulullah alimkaribisha, akamkirimu, na kumtandikia kitamba chake cha baraka ili akae. Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) akamuombea dua Maalum kwa ajili yake akisema, “Ewe Mwenyezi Mungu! Mjalie waail na baraka, na watoto zake na wajukuu. ” Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) akamchagua kama naibu wake juu ya watu wa Yemen.

Kabla ya kuondoka kutoka Madinah Munawwarah, alimuomba Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) ampe ardhi huko Yemen. Kwa ombi lake, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alimchagulia kiwanja cha Yemen, na akamwagiza Mu’aawiyah (Radhiyallahu anhu) aende naye Yemen ili am amkatie kiwanja chake na kumkabidhi.

Ipasavyo, waa’il na Mu’aawiyah (Radhiyallahu anhuma) aliondoka pamoja kutoka Madinah Munawwarah. Waa’l (Radhiyallahu anhu) alikuwa akisafiri kwenye ngamia, wakati Mu’aawiyah(Radhiyallahu anhu) alikuwa akisafiri kwa miguu. Wakati huo, Mu’aawiyah (Radhiyallahu anhu) alikuwa masikini sana hata hakuwa na viatu vya kuvaa kufunika miguu yake wakati wa safari.

About admin

Check Also

Kuwa Na Wasiwasi Juu ya Elimu ya Dini ya mtoto

Taifa lililobarikiwa na maarifa ya Dini na uelewa mzuri ni taifa linaloendelea na lenye msimamo …