Ukarimu Na Zuhd (Kujiepusha na dunia) Wa Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Wakati mmoja, Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) alichukua sarafu za dhahabu mia nne, akaziweka kwenye mfuko na akampa mtumishi wake akisema, “Nenda kwa Abu Ubaidah (Radhiyallahu ‘anhu) na umpe fedha hizi. Baada ya hapo, kaa hapo kwa muda ili kuona atafanya nini na pesa (na urudi kunijulisha).”

Mtumishi alichukua mfuko wa sarafu za dhahabu na akaenda kwa Abu Ubaidah (Radhiyallahu ‘anhu). Akaampa zawadi akisema, “Ameerul Mu-mineen amesema kwamba unapaswa kutumia hizi kwa mahitaji yako.”

Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu) aliipokea zawadi hiyo na akamuombea dua Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) akisema, “Allah Ta’ala amjaalie ukaribu Wake maalum na amrehemu”.

Kisha akamwita mjakazi wake na kutoa sarafu chache za dhahabu kutoka kwenye mfuko na kusema, “Chukua sarafu hizi saba za dhahabu na umpe mtu fulani.” Kisha akatoa chache zaidi na kusema, “Toa hizi tano
sarafu za dhahabu kwa mtu fulani.” Aliendelea kutoa sarafu za dhahabu kwenye begi na kutoa na kuumpa mtumishi wake, akamwamuru awape watu mbalimbali mpaka dhahabu zote ziishe.

Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) aliposikia jinsi Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu) alivyozitumia pesa hizo kwa waja wa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’alah) katika sadaka, alifurahishwa sana. (Al-Mu’jamul Kabiir #46)

About admin

Check Also

Tamaa Ya Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) Kubarikiwa Na Chumba Kilichojaa Na Watu Kama Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) wakati fulani alikua amekaa pamoja na kundi la watu alipokuwa akiwahutubia …