Sunnat Na Adabu Za Kuamkiana (Kutoa Salaam) 1

1. Unapokutana na ndugu yako Muislamu, muamkie kwa kutoa salaam.

Ali (Radhiya Allaahu ‘anhu) anaripoti kwamba Mtume (sallallahu alaihi wasallam) alisema, “Muislamu ana haki sita juu ya ndugu yake Mwislamu. Akikutana naye amsalimie (kwa kutoa salaam); akimwalika, akubali mwaliko wake; anapotoa chafya (na kusema alhamdulillah), ajibu chafya yake kwa kusema ‘Yarhamukallah’; anapoumwa mgonjwa, amtembelee; akifariki ahudhurie janaazah yake; na anapaswa kumpendelea kile anachopenda kwa ajili yake mwenyewe.”[1]

2. Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) ametuhimiza katika hadith kufanya salaam kuwa ni jambo la kawaida miongoni mwetu. Kutoa salaam itakuwa ni njia ya kujenga upendo na umoja kati yetu.

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraira (radhiyallahu ‘anhu) kwamba Mtume (sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Hamtaingia Peponi mpaka mlete Imaan, na huwezi kupata Imaan kamili mpaka mmiliki upendo baina yenu. Je, niwaonyeshe jinsi ya kuwa na upendo kati yenu? Fanyeni salaam kuwa ni jambo la kawaida baina yenu (wakati wa kukutana).”[2]

3. Sunnah ya salaam ni kuwasalimia Waislamu wote, sio tu familia ya mtu, marafiki na watu unaowajua.

Abdullah bin Amr (Radhiyallahu ‘anhu) anasimulia kwamba mtu mmoja aliwahi kumuuliza Mtume (sallallahu alaihi wasallam):
“Ni kipengele gani na adabu gani ya Uislamu ni ya kusifiwa sana na yenye thawabu?” Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) akajibu: “Kulisha viumbe na kuwatolea salamu watu, ukiwa unawajua au huwajui.”[3]


[1] سنن الترمذي، الرقم: 2736، وقال: هذا حديث حسن

[2] صحيح مسلم، الرقم: 54

[3] صحيح البخاري، الرقم: 12

About admin

Check Also

Sunnah Na Adabu Za Kuwatembelea Marehemu 4

14. Wasaidie waliofiwa kwa kuwapelekea chakula nyumbani kwao. Mtume (Sallallahu ‘alaihi wasallam) amewafundisha Maswahaba (radhiyallahu …