Katika malezi ya mtoto, ni muhimu sana kwa wazazi kuhakikisha kuwa mtoto wao daima anakua katika mazingura ya wacha mungu na huwekwa wazi kwa mazingira mazuri.
Mazingira mazuri na ushirika wa dini yataacha hisia kubwa juu ya moyo wa mtoto ambayo baadaye itaunda mawazo yake na kuunda mtazamo wake katika maisha.
Kama matokeo, mtoto atakua na mawazo sahihi ya Uislamu na moyo wake utaundwa na maadili ya kweli ya Uislamu.
Hadith inaelezea kuwa kila mtoto huzaliwa na tabia safi. Mtazamo huu utamwezesha kuona na kuelewa ukweli wa Uislamu wakati anakua. Lakini, kupitia mtoto kuwa katika mazingira yasiyofaa, mtoto hushawishiwa kuelekea katika dini mbaya. Ndo mana, mtoto aliyezaliwa katika nyumba ya Myahudi, Mkristo, au mwabudu-moto anachukua dini ya wazazi wake.
Faida Na Madhara Ya Mazingira Mazuri Na Mabaya
Katika Hadith moja, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alilinganisha rafiki wa dini na mtu aliyebeba musk (manukato), na alilinganisha rafiki mbaya na mtu anayeshangaza moto.
Rasulullah aligundua kuwa kupitia kubaki katika mazingira ya muuza musk, hata ikiwa mtu hatapokea musk kama zawadi au kununua musk kutoka kwake, basi kwa uchache sana, atafaidika na harufu nzuri ya musk wakati amebaki katika kampuni yake.
Kinyume chake, kupitia kubaki katika mazingira ya mtu anayechochea moto, hata ikiwa mavazi ya mtu hayakuchomwa na moto, bado ataathiriwa na moto kupitia harufu mbaya ya moshi.
Katika Hadith hii, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alieleza kwamba kubaki katika mazingira mazuri haitakuso kuwa na faida, na vili vile kubaki katika mazingira mabaya haitakosa kuwa na madhara.
Tunaposoma maisha ya maswahaabah (Radhiyallahu anhum), tunaona kwamba walielewa kuwa mazingira ya mtu ina athari kubwa juu yake. Kwa hivyo, kuna matukio mengi ambayo yanaonyesha wasiwasi ambao maswahaabah (Radhiyallahu anhum) walikuwa nao kwa watoto wao kubaki katika mazingira mazuri na ya kidini.
Chini ni matukio mawili ambayo yanaonyesha wasiwasi mkubwa ambao Maswahaabah (Radhiyallahu anhum) walikuwa nao kwa watoto zao kubaki katika kampuni ya dini na kupata faida ya Dini.
Ummu Sulaim Akiwa Na Wasiwasi Na Mtoto Wake
Inaripotiwa kwamba wakati Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alifanya Hijrah na akaja Madinah Munawwarah, Anas (Radhiyallahu anhu) alikuwa na kijana mdogo ambaye alikuwa na umri wa miaka nane tu. Baada ya kufika kwa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam), mama yake alimshika mkono na kumpeleka kwa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam).
Walipofika mbele ya Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam), mama wa Anas (Radhiyallahu anhu) alimuambia Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam), “Ewe Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam)! Hakuna mwanaume au mwanamke wa Ansaar ambaye hajakuletea zawadi. Lakini, sina chochote cha kukuletea kama zawadi badala ya mwanangu. Kwa hivyo, tafadhali umkubali awe katika huduma yako.”
Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alimkubali katika huduma yake, na akabaki katika mazingira yaliyobarikiwa ya Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) kwa miaka kumi.
Mama wa Anas (Radhiyallahu anhu), Ummu Sulaim(Radhiyallahu anha), alielewa thamani ya mazingira mazuri. Kwa kuwa hakuwezi kuwa na mazingira bora kuliko kampuni ya Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam), alitaka mtoto wake mdogo abaki katika kampuni yake iliyobarikiwa.
Abbaas (Radhiyallahu anhu) Akiwa na wasiwasi juu ya mtoto wake
Abbaas (Radhiyallahu anhu), mjomba wa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam), alitaka mtoto wake, Abdullah bin Abbaas (Radhiyallahu anhuma), apate baraka maalum kupitia kubaki katika mazingira yaliyobarikiwa na Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam).
Kwa hivyo, inaripotiwa kutoka kwa Abdullah bin Abbaas (Radhiyallahu anhuma) kwamba wakati alikuwa kijana, takriban miaka kumi na mbili au kumi na tatu, baba yake, Abbaas (Radhiyallahu anhu), alimwagiza akeshe usiku nyumbani kwa shangazi yake, Maimoonah (Radhiyallahu anha), ili kufaidika na Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) na achunguze Salaah ya Tahajjud ya mtume (Sallallahu alaihi wasallam).
Ipasavyo, Ibnu Abbaas (Radhiyallahu anhuma) alikesha usiku wake Nyumbani kwa shangazi yake, akiangalia Tahajjud ya Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam), na baadaye akawafikishia ummah jinsi Rasulullah alivyo swali Tahajjud.
Kampuni sio tu kwa ushirika wa kimwili
Wakati watu wanafikiria juu ya kampuni na ushirika, kwa ujumla ni marafiki na urafiki wa mwili ambao huja akilini. Lakini, neno ‘kampuni’ na ‘uhusiano’ yana maana pana zaidi. Kwa asili, kila kitu katika mazingira ambayo hushawishi fikira za mtu, huunda mawazo ya mtu na kuathiri tabia na mwenendo wa mtu inaweza kuzingatiwa kama kampuni na ushirika.
Kwa hivyo, maandishi ambayo mtu anasoma, websites ambavyo ata tafuta, akaunti kwenye social media ambayo mtu anafuata, nk – haya yote ni aina tofauti za kampuni na ushirika ambao huunda mawazo ya mtu na kushawishi na kuunda malengo ya mtu.
Kwa hivyo, kama vile ni muhimu kwa wazazi kuwa makini na kugundua kuhusu marafiki ya watoto zao, ni muhimu pia
kwao kufuatilia kwa karibu na kudhibiti vitu vingine vya mazingira ambayo watoto wao hudhihirishwa.