Katika malezi ya mtoto, ni muhimu sana kwa wazazi kuhakikisha kuwa mtoto wao daima anakua katika mazingura ya wacha mungu na huwekwa wazi kwa mazingira mazuri.
Mazingira mazuri na ushirika wa dini yataacha hisia kubwa juu ya moyo wa mtoto ambayo baadaye itaunda mawazo yake na kuunda mtazamo wake katika maisha.
Kama matokeo, mtoto atakua na mawazo sahihi ya Uislamu na moyo wake utaundwa na maadili ya kweli ya Uislamu.
Hadith inaelezea kuwa kila mtoto huzaliwa na tabia safi. Mtazamo huu utamwezesha kuona na kuelewa ukweli wa Uislamu wakati anakua. Lakini, kupitia mtoto kuwa katika mazingira yasiyofaa, mtoto hushawishiwa kuelekea katika dini mbaya. Ndo mana, mtoto aliyezaliwa katika nyumba ya Myahudi, Mkristo, au mwabudu-moto anachukua dini ya wazazi wake.
Faida Na Madhara Ya Mazingira Mazuri Na Mabaya
Katika Hadith moja, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alilinganisha rafiki wa dini na mtu aliyebeba musk (manukato), na alilinganisha rafiki mbaya na mtu anayeshangaza moto.
Rasulullah aligundua kuwa kupitia kubaki katika mazingira ya muuza musk, hata ikiwa mtu hatapokea musk kama zawadi au kununua musk kutoka kwake, basi kwa uchache sana, atafaidika na harufu nzuri ya musk wakati amebaki katika kampuni yake.
Kinyume chake, kupitia kubaki katika mazingira ya mtu anayechochea moto, hata ikiwa mavazi ya mtu hayakuchomwa na moto, bado ataathiriwa na moto kupitia harufu mbaya ya moshi.
Katika Hadith hii, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alieleza kwamba kubaki katika mazingira mazuri haitakuso kuwa na faida, na vili vile kubaki katika mazingira mabaya haitakosa kuwa na madhara.
Tunaposoma maisha ya maswahaabah (Radhiyallahu anhum), tunaona kwamba walielewa kuwa mazingira ya mtu ina athari kubwa juu yake. Kwa hivyo, kuna matukio mengi ambayo yanaonyesha wasiwasi ambao maswahaabah (Radhiyallahu anhum) walikuwa nao kwa watoto wao kubaki katika mazingira mazuri na ya kidini.
Chini ni matukio mawili ambayo yanaonyesha wasiwasi mkubwa ambao Maswahaabah (Radhiyallahu anhum) walikuwa nao kwa watoto zao kubaki katika kampuni ya dini na kupata faida ya Dini.