Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu kula haramu na kujihusisha na madhambi inazuia dua kujibiwa. Imepokewa kutoka kwa Abu Huraira (radhiyallahu ‘anhu) kwamba Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) amesema: “Enyi watu, hakika Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’aala) ni Msafi na anakubali kilicho safi. …

Soma Zaidi »

Maisha Ya Uislamu

Wakati mtu anazama na kujitahidi kuishi, atafanya chochote kuokoa maisha yake. Ikiwa ana uwezo wa kukamata kamba karibu na njia ambayo anaweza kujiondoa kutoka ndani ya maji, atashikamana nayo kwa bidii na kuiona kama njia yake ya kuokoa maisha yake. Katika ulimwengu huu, muumini anapokabiliwa na mawimbi ya fitna ambayo …

Soma Zaidi »

Mshale Wa Kwanza Kurushwa kwa Ajili Ya Uislamu

Sa’d (radhiya allaahu ‘anhu) alikuwa miongoni la kundi la Maswahabah ambao Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) aliwatuma katika mwaka wa kwanza baada ya Hijrah kuuzuia msafara wa Maquraishi. Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alimteua Ubaidah bin Haarith (radhiya allaahu ‘anhu) kuwa Amir (kiongozi) wa kundi hili. Katika msafara huu, Maswahabah (radhiyallahu ‘anhum) …

Soma Zaidi »

Tafseer Ya Surah Faatihah

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ ‎﴿١﴾‏ الْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ‎﴿٢﴾‏ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ ‎﴿٣﴾‏ مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ ‎﴿٤﴾‏ إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ ‎﴿٥﴾‏ اهْدِنَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ ‎﴿٦﴾‏ صِرَاطَ الَّذِينَ أَنْعَمْتَ عَلَيْهِمْ غَيْرِ الْمَغْضُوبِ عَلَيْهِمْ وَلَا الضَّالِّينَ ‎﴿٧﴾‏ Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa ulimwengu wote. Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu. Mfalme wa Siku ya kuhukumu. Wewe peke yako tunakuabudu, na Wewe …

Soma Zaidi »

Sunna Na Adabu Za Dua 7

17. Ni bora kuomba dua pana. Aaishah (radhiyallahu ‘anha) anaripoti kwamba Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) alikuwa akipendelea dua hizo ambazo ni pana na alikuwa akiacha dua zingine. Dua hizi zifuatayo ni miongoni mwa dua za Masnoon ambazo zimepokelewa katika Hadith: رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ …

Soma Zaidi »

Damu Ya Kwanza iliyomwagika kwa ajili ya Uislamu

Muhammad bin Ishaaq (rahimahullah) anasimulia: Mwanzoni katika Uislamu, Maswahaabah wa Mtume (Sallallahu ‘alaihi wasallam) walikuwa wakiswali kwa siri. Walikuwa wakienda kwenye mabonde ya Makka Mukarramah kuswali ili Swalah zao zibaki siri kwa makafiri (na ili waokoke na mateso ya makafiri). Wakati mmoja, wakati Sa’d (Radhiya Allaahu ‘anhu) alikuwepo pamoja na …

Soma Zaidi »

Sunna Na Adabu Za Dua 6

15. Usiombe dua kwa jambo lolote lisiloruhusiwa au kwa chochote kisichowezekana (kama mtu kuomba kuwa Nabi). Imepokewa kutoka kwa Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) kwamba Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) amesema: “Dua ya mtu itakubaliwa daima maadamu haombi kitu cha dhambi au kukata mahusiano ya kifamilia, na maadamu hana haraka (katika dua …

Soma Zaidi »

Uislamu Unakaribisha Nini?

Katika zama za Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam), watu mbalimbali walianza kusilimu. Ujumbe wa Uislamu ulipoenea na kufikia maeneo mbalimbali, Aksam bin Saifi (rahimahullah), kiongozi wa ukoo wa Tameem, alipendezwa na kujua kuhusu Uislamu. Kwa hiyo, aliwatuma watu wawili kutoka katika kabila lake kusafiri kwenda Madinah Munawwarah ili kufanya utafiti kuhusu …

Soma Zaidi »

Upendo Kwa Answaar

‘Aamir (rahimahullah), mtoto wa Sa’d (radhiya allaahu ‘anhu), anasimulia yafuatayo: Wakati fulani nilimwambia baba yangu, “Ewe baba yangu mpendwa! Ninaona kwamba unaonyesha upendo na heshima ya ziada kwa Answaar ikilinganishwa na watu wengine.” Sa’d (radhiya allaahu ‘anhu) akaniuliza, “Ewe mwanangu! Hujafurahishwa na hili?” Nikamjibu, “Hapana! Sina furaha. Lakini, nimefurahishwa sana …

Soma Zaidi »

Sunna Na Adabu Za Dua 5

12. Baada ya kumaliza dua yako, sema aameen. Abu Musabbih Al-Maqraaiy anasimulia: Wakati mmoja, tulikuwa tumekaa na Abu Zuhair An-Numairi ambaye alikuwa miongoni mwa maswahaabah (radhiyallahu anhum). Alikuwa mfasaha zaidi katika lugha. Wakati mtu yoyote miongoni mwetu alikuwa akishiriki katika dua, alikuwa akisema: “ufunge dua hiyo kwa Aamin, kwa sababu …

Soma Zaidi »