{"id":2665,"date":"2024-09-24T06:16:13","date_gmt":"2024-09-24T04:16:13","guid":{"rendered":"https:\/\/sw.alislaam.com\/?p=2665"},"modified":"2024-11-05T11:04:09","modified_gmt":"2024-11-05T09:04:09","slug":"fadhila-kubwa-ya-wazazi","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/sw.alislaam.com\/?p=2665","title":{"rendered":"Fadhila Kubwa Ya Wazazi"},"content":{"rendered":"<p>Miongoni mwa neema kubwa za Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aalah) juu ya mtu ni neema ya wazazi. Neema ya wazazi ni neema yenye thamani sana na isiyoweza kubadilishwa hadi kwamba inapewa kwa mtu mara moja tu katika maisha yake.<\/p>\n<p>Kama vile neema za zingine za maisha inatolewa mara moja tu kwa mtu, na itakapoisha, haitarudi tena, hivyo ndivyo neema ya wazazi pia ipo, ikichukuliwa, haiwezi kupatikana tena.<\/p>\n<p>Kila neema ambayo mtu anafurahia ina haki fulani zinazohusiana nayo. Iwapo fadhila za wazazi ni miongoni mwa neema kubwa, basi haki zinazoambatanishwa nayo ni miongoni mwa haki muhimu sana katika dini.<\/p>\n<p>Ndani ya Quran Majeed na Hadith za mtume (sallallahu alaihi wasallam) zimejaa maamrisho kuhusu umuhimu mkubwa wa<br \/>\nkutimiza haki za wazazi na kuwatendea wema wa hali ya juu.<\/p>\n<p>Katika Qur\u2019aan Majeed, Allah Ta\u2019ala Anasema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u0648\u064e\u0642\u064e\u0636\u064e\u0649\u0670 \u0631\u064e\u0628\u0651\u064f\u0643\u064e \u0623\u064e\u0644\u0651\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0639\u0652\u0628\u064f\u062f\u064f\u0648\u0627 \u0625\u0650\u0644\u0651\u064e\u0627 \u0625\u0650\u064a\u0651\u064e\u0627\u0647\u064f \u0648\u064e\u0628\u0650\u0627\u0644\u0652\u0648\u064e\u0627\u0644\u0650\u062f\u064e\u064a\u0652\u0646\u0650 \u0625\u0650\u062d\u0652\u0633\u064e\u0627\u0646\u064b\u0627<span class=\"sign\">\u00a0\u06da<\/span>\u00a0\u0625\u0650\u0645\u0651\u064e\u0627 \u064a\u064e\u0628\u0652\u0644\u064f\u063a\u064e\u0646\u0651\u064e \u0639\u0650\u0646\u062f\u064e\u0643\u064e \u0627\u0644\u0652\u0643\u0650\u0628\u064e\u0631\u064e \u0623\u064e\u062d\u064e\u062f\u064f\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0623\u064e\u0648\u0652 \u0643\u0650\u0644\u064e\u0627\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0641\u064e\u0644\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0642\u064f\u0644 \u0644\u0651\u064e\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0623\u064f\u0641\u0651\u064d \u0648\u064e\u0644\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0646\u0652\u0647\u064e\u0631\u0652\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0648\u064e\u0642\u064f\u0644 \u0644\u0651\u064e\u0647\u064f\u0645\u064e\u0627 \u0642\u064e\u0648\u0652\u0644\u064b\u0627 \u0643\u064e\u0631\u0650\u064a\u0645\u064b\u0627\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0662\u0663\ufd3e<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Mola wako amefaradhisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na muwatendee wema wazazi wawili. Ikiwa mmoja wao au wote wawili watafikia uzee, usimwambie &#8220;Uff (neno au maneno ya hasira au maneno ya kukera)&#8221; na usiwakemee, na uongee nao kwa maneno ya heshima.<\/em><\/p>\n<p>Imepokewa katika Hadith kwamba radhi za Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;alah) ziko katika radhi za wazazi, na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;alah) iko katika kuwachukiza wazazi.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2665-1\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/09\/AUD-20240903-WA0004.mp3?_=1\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/09\/AUD-20240903-WA0004.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/09\/AUD-20240903-WA0004.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Wazazi Wako Ni Pepo Au Jahannum Yako<\/strong><\/p>\n<p>Wakati fulani, Sahaabi alimuuliza Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) kuhusu haki za wazazi. Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) akasema: &#8220;Hao (wazazi) ni Pepo yako au Jahannamu yako.&#8221;<\/p>\n<p>Kwa maneno mengine, ikiwa mtu ni mpole, mwenye huruma na upendo kwa wazazi wake na kuwatii katika mambo yote yanayoruhusiwa, atabarikiwa na Jannah. Kinyume chake, ikiwa atawaasi na akawa mkali na mkorofi kwao, basi matendo yake mabaya yatakuwa sababu ya yeye kuingia katika moto wa Jahannamu.<\/p>\n<p><strong>Milango Miwili Ya Jannah Ikibaki wazi<\/strong><\/p>\n<p>Katika Hadith nyingine, Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: \u201cMuislamu yoyote atakaepitisha siku yake katika hali ya kuwa wazazi wake wameridhika naye (yaani anamtii Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;alah) katika kutekeleza haki za wazazi wake), basi milango miwili ya Jannah itafunguliwa kwa ajili yake. Ikiwa ana mzazi mmoja tu aliye hai, basi mlango mmoja tu utakuwa wazi kwa ajili yake.<\/p>\n<p>\u201cMuislamu yoyote anayepitisha siku yake katika hali ya kuwa wazazi wake wamemkasirikia (yaani kumuasi Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;alah) katika kutekeleza haki za wazazi wake), basi milango miwili ya Jahannam yatafunguliwa kwa ajili yake. Ikiwa ana mzazi mmoja tu aliye hai, basi mlango mmoja tu utakuwa wazi kwa ajili yake.\u201d<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2665-2\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/09\/AUD-20240910-WA0008.mp3?_=2\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/09\/AUD-20240910-WA0008.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/09\/AUD-20240910-WA0008.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Tukio La Mwanaume Kumbeba Mama Yake Wakati Wa Kufanya Thawaaf<\/strong><\/p>\n<p>Imepokewa kwamba katika tukio moja, Abdullah bin Umar (radhiyallahu anhuma) alikuwa akifanya thawaaf alipomuona mtu kutoka Yemen akiwa amembeba mama yake mgongoni huku akifanya thawaaf.<\/p>\n<p>Mwanaume huyo akiwa amembeba, alikuwa akitamka maneno yafuatayo kama mashairi:<\/p>\n<p>Mimi ni ngamia wake mtiifu. Usafiri mwingine wowote ambao anaweza kupanda unaweza kumuogopesha, lakini kamwe sitamsababishia hofu yoyote (yaani, sitamsababishia usumbufu wowote). Sasa nimembeba mgongoni, lakini kipindi alichonibeba tumboni mwake kilikuwa kirefu zaidi.<\/p>\n<p>Baada ya kumaliza thawaaf, mtu huyo alimuuliza Ibnu Umar (radhiyallahu anhuma), \u201cJe, nimetimiza haki ya mama yangu kwa kumbeba wakati wa thawaaf?\u201d<\/p>\n<p>Ibnu Umar (radhiyallahu anhuma) akajibu, \u201cHapana! Kwa kweli, hujamlipa hata dakika moja ya maumivu aliyopata wakati wa kukuzaa wewe.\u201d<\/p>\n<p>Utiifu na huduma kwa wazazi ni njia inayoelekea Jannah. Kuona faraja ya wazazi, kuwatimizia haja zao na kuwaonyesha upendo na heshima wanayostahiki ni ibaadah kubwa inayompa mtu thawabu kubwa katika dunia hii na ijayo.<\/p>\n<p><strong>Malipo Ya Hajj Iliyokubaliwa<\/strong><\/p>\n<p>Imepokewa kutoka kwa Abdullah bin Abbaas (radhiyallahu anhuma) kwamba Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: \u201cHakuna mtoto mtiifu anayewatazama wazazi wake kwa huruma (na mapenzi) isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta\u2019ala) anamuandikia malipo ya hajj iliyokubaliwa kwa kila anapowatazama wazazi wake kwa huruma)&#8221;<\/p>\n<p>Maswahaaba (radhiyallahu anhum) wakauliza, \u201cHata kama anatazama mara mia moja kila siku?\u201d Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) akajibu: \u201cNdiyo, Allah (Ta&#8217;ala) ni mkubwa zaidi na Yeye ni Mkarimu zaidi (malipo yake ni mengi kuliko vile unavyodhania).\u201d<\/p>\n<p><strong>Kuto Kuleta Usumbufu kwa Wazazi<\/strong><\/p>\n<p>Ikiwa tunafurahisha mioyo ya wazazi wetu, watatupa dua zao za dhati ambazo zitatusaidia katika dunia hii na ijayo. Kinyume chake, kuwapuuza wazazi wetu na kuumiza nyoyo zao ni dhambi kali ambayo itatunyima wema wote, furaha na baraka katika maisha yetu.<\/p>\n<p>Zaidi ya hayo, imeripotiwa kwamba yule ambaye anawakosea adabu wazazi wake na kuwa na tabia mbaya ataadhibiwa katika dunia hii, na pia adhabu ataipata Akhera.<\/p>\n<p>Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: \u201cAllah Ta\u2019ala atasamehe dhambi yoyote anayoitaka, kasoro dhambi ya kuwaasi wazazi wake (yaani Allah Ta\u2019ala kawaida hasamehe dhambi hii bila ya mtu kuomba msamaha kwa wazazi wake).<\/p>\n<p>\u201cHakika Allah Ta\u2019ala atamuadhibu mtu katika dunia hii kabla ya kuondoka duniani (yaani ukitoa adhabu iliyohifadhiwa kwake<br \/>\nakhera kwa kuwaudhi wazazi wake, ataadhibiwa pia katika ulimwengu huu).<\/p>\n<p>Hata hivyo, ni muhimu kukumbuka kwamba ikiwa wazazi wa mtu wanataka mtu afanye jambo kinyume na shari\u2019ah, basi ni lazima kwa heshima ajiepushe na vitendo hivyo, kwa sababu utiifu wa Allah Ta\u2019ala ndio kipaumbele cha kwanza.<\/p>\n<p><strong>Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) Akimhudumia Mama Yake<\/strong><\/p>\n<p>Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) ni Sahaabi maarufu miongoni mwa Maswahaba Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam). Alisilimu katika mwaka wa 7 A.H. na akabaki na Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) hadi mwisho wa maisha yake. Ingawa alikaa miaka michache tu na Mtume (Sallallahu alaihi wasallam), Allah Ta\u2019ala alimbariki kwa heshima ya kupokea hadith kiasi kikubwa zaidi kutoka kwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam).<\/p>\n<p>Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) alikuwa akibaki daima katika huduma ya mama yake ambaye alikuwa mzee na alihitaji huduma yake. Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) alikuwa amemuamuru abakie katika khidmat ya mama yake mzee.<\/p>\n<p>Imepokewa kwamba katika tukio la Vita vya Khaibar, Mtume (sallallahu alaihi wasallam) aliwahutubia Maswahaba na akawahimiza kushiriki katika jihaad. Kusikia haya, Maswahabah (radhiyallahu anhum) mara moja wakaharakisha kujiandaa kwa ajili ya jihaad.<\/p>\n<p>Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) alikuwa na shauku pia ya kushiriki katika kampeni na kupigana jihaad upande wa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam). Lakini, mama yake alihitaji usaidizi wake na khidmah yake. Kwa hiyo, alikwenda kwa mama yake na kusema: \u201cTafadhali niruhusu nijitayarishe na niende kwa ajili ya jihaad, kwa sababu Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amewaamrisha Maswahaba (radhiyallahu anhum) kujiandaa na kutoka kwenda jihaad.<\/p>\n<p>Kusikia hivyo, mama yake hakufurahi na akasema, \u201cUnawezaje kwenda wakati unajua ugumu nitakaoupata wakati haupo hapa?\u201d Hata hivyo, kutokana na shauku yake ya kujiunga na Rasulullah, alisisitiza kusema, \u201cSiwezi kubaki nyuma na kutengwa na Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam)!<\/p>\n<p>Mama yake alizidi kumsihi na hata kumkumbusha haki yake juu yake kwa sababu ya kumlea na kumnyonyesha utotoni, lakini alionekana amedhamiria kuungana na Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam).<\/p>\n<p>Mama yake Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) hivyo alikuja kwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) kwa siri na kumjulisha yaliyotokea. Alieleza kuwa mwanawe alikuwa na hamu ya kujiunga na safari, lakini alihitaji khidmah yake nyumbani. Baada ya kusikiliza malalamiko yake, Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) alisema, \u201cUnaweza kwenda, kwa sababu hitaji lako litashughulikiwa.\u201d<\/p>\n<p>Baada ya hapo, pale Abu Hurairah alipokuja kwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam), Mtume (sallallahu alaihi wasallam) alijitenga naye. Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) hapo hapo akatambua kwamba Mtume (sallallahu alaihi wasallam) amemkasirikia na hivyo akasema: \u201cEwe Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam)! Ninaona kwamba unageuza uso wako kutoka kwangu, na Ninajua kuwa wewe kutokunifurahia kunaweza tu kuwa kwa sababu ya baadhi ya malalamiko uliyoyasikia kunihusu mimi.\u201d<\/p>\n<p>Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) akamwambia, \u201cJe, wewe ni yule ambaye mama yake analazimika kumsihi, kiasi kwamba inamlazimu hata kumkumbusha haqq yake juu yake ya kumnyonyesha! Je, unapokuwa katika huduma ya wazazi wako, unafikiri kwamba wewe hauko katika njia ya Allah Ta\u2019ala? Bali mtu anapowafanyia wema wazazi wake na kutimiza haki zao, basi yeye yuko katika Njia ya Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<p>Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) hivyo alibaki nyumbani na mama yake na hakujiunga na msafara. Kwa hakika, Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) alisema baadae, \u201cKwa muda wa miaka miwili iliyofuata, hadi kifo cha mama yangu, nilibaki naye, katika utumishi wake, na sikujiunga na msafara wowote wa jihaad.\u201d<\/p>\n<p>Kutokana na Hadith hii tunaelewa malipo makubwa atakayopata mtu kwa kujishughulisha na khidmah ya wazazi wake.<\/p>\n<p><strong>Haki Kumi Na Nne Za Wazazi<\/strong><\/p>\n<p>Moulana Abraarul Haqq Saheb ametaja nukta 14 kuhusu haki za wazazi (nukta 7 ni kuhusu kutimiza haki zao wakati wa uhai wao na nukta 7 ni kuhusu kutimiza haki zao baada ya kufariki kwao).<\/p>\n<p>Haki Saba katika Maisha yao<\/p>\n<p>1. Adhmah: Kuwaheshimu.<\/p>\n<p>2. Muhabbah: Kuwa na mapenzi ya dhati kwao.<\/p>\n<p>3. Itaa\u2019ah: Kuwatii.<\/p>\n<p>4. Khidmat: Kuwahudumia.<\/p>\n<p>5. Fikr-ul-Raahah: Kuwafanyiya wepesi na faraja.<\/p>\n<p>6. Raf-ul-Haajah: Kushughulikia mahitaji yao yote.<\/p>\n<p>7. Kuwatembelea mara kwa mara.<\/p>\n<p><strong>Haki Saba baada ya Kufariki kwao.<\/strong><\/p>\n<p>1. Dua-ul-Maghfirah: Kumwomba Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;alah) Msamaha kwao na kuwamiminia rehma zake maalum juu yao.<\/p>\n<p>2. Esaal-ul-thawaab: Kuwafikishia mara kwa mara thawaab kwao (kwa kutoa sadaqah, kufanya ibaadah ya nafl, n.k. na kufikisha ujira kwao)<\/p>\n<p>3. Ikraam-ul-A\u2019izzah wa Ahbaab wa Ahl-ul-Qaraabat: Kuwaheshimu jamaa, marafiki na washirika wao.<\/p>\n<p>4. I\u2019aanat-ul-A\u2019izzah wa Ahbaab wa Ahl-ul-Qaraabat: Kuwasaidie jamaa, marafiki na washirika wao kulingana na uwezo wako.<\/p>\n<p>5. Adaa-ul-Dain wa Amaanah: Kulipa madeni yao na kurudisha amaanah yoyote.<\/p>\n<p>6. Tanfeedh-ul-Jaaiz Wasiyyah: Kutekeleza wasia wao yakihalali.<\/p>\n<p>7. Kutembelea makaburi yao mara kwa mara.<\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>Miongoni mwa neema kubwa za Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aalah) juu ya mtu ni neema ya wazazi. Neema ya wazazi ni neema yenye thamani sana na isiyoweza kubadilishwa hadi kwamba inapewa kwa mtu mara moja tu katika maisha yake. Kama vile neema za zingine za maisha inatolewa mara moja tu kwa mtu, na itakapoisha, haitarudi tena, &hellip;<\/p>\n","protected":false},"author":4,"featured_media":1910,"comment_status":"closed","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"footnotes":""},"categories":[29],"tags":[],"class_list":["post-2665","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","","category-bustani-ya-mapenzi"],"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/2665","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/users\/4"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcomments&post=2665"}],"version-history":[{"count":10,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/2665\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":2690,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/2665\/revisions\/2690"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/media\/1910"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fmedia&parent=2665"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcategories&post=2665"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Ftags&post=2665"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}