{"id":2288,"date":"2024-09-14T06:29:59","date_gmt":"2024-09-14T04:29:59","guid":{"rendered":"https:\/\/sw.alislaam.com\/?p=2288"},"modified":"2024-11-02T07:14:03","modified_gmt":"2024-11-02T05:14:03","slug":"2288","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/sw.alislaam.com\/?p=2288","title":{"rendered":"Tafseer Ya Surah Faatihah"},"content":{"rendered":"<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\"><span id=\"1-1\" class=\"aya selected\">\u0628\u0650\u0633\u0652\u0645\u0650 \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0652\u0645\u064e\u0670\u0646\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0650\u064a\u0645\u0650\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0661\ufd3e\u200f<\/span><\/span>\u00a0<span id=\"1-2\" class=\"aya\">\u0627\u0644\u0652\u062d\u064e\u0645\u0652\u062f\u064f \u0644\u0650\u0644\u0651\u064e\u0647\u0650 \u0631\u064e\u0628\u0651\u0650 \u0627\u0644\u0652\u0639\u064e\u0627\u0644\u064e\u0645\u0650\u064a\u0646\u064e\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0662\ufd3e\u200f<\/span><\/span>\u00a0<span id=\"1-3\" class=\"aya\">\u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0652\u0645\u064e\u0670\u0646\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0650\u064a\u0645\u0650\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0663\ufd3e\u200f<\/span><\/span>\u00a0<span id=\"1-4\" class=\"aya\">\u0645\u064e\u0627\u0644\u0650\u0643\u0650 \u064a\u064e\u0648\u0652\u0645\u0650 \u0627\u0644\u062f\u0651\u0650\u064a\u0646\u0650\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0664\ufd3e\u200f<\/span><\/span>\u00a0<span id=\"1-5\" class=\"aya\">\u0625\u0650\u064a\u0651\u064e\u0627\u0643\u064e \u0646\u064e\u0639\u0652\u0628\u064f\u062f\u064f \u0648\u064e\u0625\u0650\u064a\u0651\u064e\u0627\u0643\u064e \u0646\u064e\u0633\u0652\u062a\u064e\u0639\u0650\u064a\u0646\u064f\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0665\ufd3e\u200f<\/span><\/span>\u00a0<span id=\"1-6\" class=\"aya\">\u0627\u0647\u0652\u062f\u0650\u0646\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0635\u0651\u0650\u0631\u064e\u0627\u0637\u064e \u0627\u0644\u0652\u0645\u064f\u0633\u0652\u062a\u064e\u0642\u0650\u064a\u0645\u064e\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0666\ufd3e\u200f<\/span><\/span>\u00a0<span id=\"1-7\" class=\"aya\">\u0635\u0650\u0631\u064e\u0627\u0637\u064e \u0627\u0644\u0651\u064e\u0630\u0650\u064a\u0646\u064e \u0623\u064e\u0646\u0652\u0639\u064e\u0645\u0652\u062a\u064e \u0639\u064e\u0644\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650\u0645\u0652 \u063a\u064e\u064a\u0652\u0631\u0650 \u0627\u0644\u0652\u0645\u064e\u063a\u0652\u0636\u064f\u0648\u0628\u0650 \u0639\u064e\u0644\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650\u0645\u0652 \u0648\u064e\u0644\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0636\u0651\u064e\u0627\u0644\u0651\u0650\u064a\u0646\u064e\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0667\ufd3e\u200f<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa ulimwengu wote. Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu. Mfalme wa Siku ya kuhukumu. Wewe peke yako tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada. Tuonyeshe njia iliyonyooka &#8211; njia ya wale uliowafadhilisha (kwa fadhila Yako), sio njia ya waliokasirikiwa na njia ya waliopotea.<\/em><\/p>\n<p><strong>Surah Ya Kwanza<\/strong><\/p>\n<p>Surah Faatihah ni surah ya kwanza ndani ya Qur&#8217;an Tukufu. Sio tu surah ya kwanza katika pangilio za surah ya Qur&#8217;an, lakini pia ni surah ya kwanza kuteremshwa na Allah Ta\u2018ala. Kabla ya kuteremshwa kwa Surah Faatihah, ingawa aya za mwanzo za Surah Alaq na Surah Muddathir ziliteremshwa, lakini hakuna Sura kamili iliyoteremshwa kabla yake.<\/p>\n<p>Sababu ya Surah Faatihah kuwekwa mbele ya kila Sura nyingine ya Qur&#8217;an Majeed ni kwamba Sura Faatihah ndio asili ya Qur&#8217;an Majeed, na katika mada yake, inajumuisha dhamira kuu tatu za Qur&#8217;an Majeed. Kwa hiyo, sehemu zote zingine katika Qur&#8217;an Majeed zinazofuata baada ya Surah Faatihah ni kama maelezo yake katika kufafanua mada zake kuu tatu.<\/p>\n<p><strong>Mada Tatu Kuu Za Qur&#8217;an Takatifu<\/strong><\/p>\n<p>Kimsingi, elimu iliyomo ndani ya Qur&#8217;an Takatifu yote inahusiana na mojawapo ya mada kuu tatu; (1) kuleta Imaan katika umoja wa Allah Ta\u2018ala na katika sifa Zake takatifu, (2) kutekeleza A\u2019amaal-ul-Swaalihah (amali njema), (3) maisha ya Akhera.<\/p>\n<p>Kanuni za msingi za mada zote hizi tatu kuu zimerejelewa na kuonyeshwa katika Surah Faatihah. Ni kwa sababu hii kwamba miongoni mwa majina ambayo Surah Faatihah imetolewa, kama ilivyotajwa katika Ahaadith, ni majina \u201cUmmul Qur-aan\u201d (Mama wa Qur&#8217;an), \u201cUmmul Kitaab\u201d (Mama wa Kitabu), na \u201cAl-Qur&#8217;an-ul-Adhim (Qur&#8217;an Tukufu)\u201d.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-1\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/04\/AUD-20240420-WA0007.mp3?_=1\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/04\/AUD-20240420-WA0007.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/04\/AUD-20240420-WA0007.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Ujumbe Wa Surah Faatihah<\/strong><\/p>\n<p>Mtu anapochunguza mada ya surah hii, anatambua kwamba ni ujumbe kutoka kwa Allah Ta\u2019ala kwa mwanadamu kuhusiana na jinsi anavyopaswa kumuomba Allah Ta\u2019ala na kutafuta mwongozo kutoka Kwake. Kwa hiyo, katika surah hii mtu anamuomba Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) amwonyeshe njia ya wale waliofadhiliwa na Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) na amuepushe na njia ya wale walioighadhibikiwa na njia ya waliotumia kupotea.<\/p>\n<p>Allah Ta\u2019ala anajibu dua hii ya mwanaadamu kwa kumpa muongozo ambao uliteremshwa katika Qur-aan nzima baada ya Surah hii. Kwa hivyo, ni kwamba sehemu nzima ya Qur-aan Takatifu uliosalia ni jibu kwa dua hii ya mwanadamu katika Surah Faatihah.<\/p>\n<p><strong>Mtazamo Wa Ujumbe Wa Surah Faatihah<\/strong><\/p>\n<p>Mtazamo wa ujumbe wa surah hii ni kwamba ili mtu afaidike na Quran Takatifu, anatakiwa kuleta imaan katika vipengele vya msingi vya imani k.m. (1) Kuamini umoja wa Allah Taala (2) Kuamini sifa zake zote nzuri (3) Kuamini kama kuna maisha ya akhera (4) Kuamini hisabu ya siku ya qiyama (5) Kuamini risaalah (utume) wa Rasulullah (Sallallahu &#8216;alaihi wasallam) (6) Kufuata njia ya wachamungu (Ambiyaa[\u2018alaihimus salaam]) (7) Kujiepusha na njia ya maadui wake yanayomfanya mtu kum&#8217;aasi Allah Ta&#8217;ala.<\/p>\n<p>Vile vile surah hii inamuelekeza mwanadamu katika kufikia lengo lake kwa kurejea kikamilifu kwa Allah Ta\u2019ala kwa kumuabudu yeye pekee, kuomba mwongozo na msaada kutoka Kwake.<\/p>\n<p>Iwapo mtu atasoma surah hii na akaisoma kwa akili iliyo wazi na moyo mnyofu, kama mtafutaji ukweli wa haki, bila shaka atabarikiwa na mwongozo wa kweli kutoka kwa Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-2\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/04\/AUD-20240427-WA0006.mp3?_=2\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/04\/AUD-20240427-WA0006.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/04\/AUD-20240427-WA0006.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Fadhila za Surah Fatiha<\/strong><\/p>\n<p>Kuhusiana na fadhila za Surah Faatihah Rasulullah (sallallahu &#8216;alaihi wasallam) amesema kuwa surah hii ni tiba ya kila aina ya maradhi. Kwa mujibu wa Hadith nyingine, surah hii pia inaitwa \u201cAs-Shifaa\u201d (Tiba ya Maradhi Yote).<\/p>\n<p>Imepokewa pia kutoka kwa Anas (radhiya allaahu \u2018anhu) kwamba Rasulullah (sallallahu &#8216;alaihi wasallam) ameiita surah hii kuwa ni surah kuu kati ya surah zote za Qur&#8217;an Takatifu.<\/p>\n<p>Katika Hadith nyingine, Abu Hurairah (radhiya allaahu &#8216;anhu) anasimulia kwamba Mtume (sallallahu &#8216;alaihi wasallam) amesema: &#8220;Naapa kwa Allah Ta&#8217;ala, ambaye ni Mola wa maisha yangu, kwamba si Tawrah, wala Injili wala Zabuur wala sehemu nyingine yoyote ya Qur&#8217;an inaweza kulinganishwa na Sura Faatiha.\u201d<\/p>\n<p>Maulamaa wanaeleza kwamba vitabu vya Allah Ta&#8217;ala yanafikia takriban 104, na ujumbe za vitabu hizi zote zimo katika vitabu vinne mashuhuri; Zabuur, Tawrah, Injili na Qur&#8217;an. Ujumbe mtukufu wa vitabu hivi vyote umefupishwa ndani ya Qur-aan, na ujumbe wa kimsingi wa Qur-aan umeingizwa ndani ya Surah Faatihah. Zaidi ya hayo, ujumbe wa Surah Faatihah unaweza kupatikana kwa ufupi katika maneno \u201cBismillahir Rahmaanir Raheem\u201d.<\/p>\n<p><strong>Asili Ya Bismillah<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\"><span id=\"1-1\" class=\"aya selected\">\u0628\u0650\u0633\u0652\u0645\u0650 \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0652\u0645\u064e\u0670\u0646\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0650\u064a\u0645\u0650\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0661\ufd3e<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rahma, Mwenye kurehemu<\/em><\/p>\n<p>Ilikuwa ni tabia na njia ya watu katika zama ya kabla ya Uislamu kwamba wanapoanza kazi yoyote au kuanza mradi wowote, walichukua majina ya masanamu yao ili kupata baraka. Allah Ta\u2019ala alivifuta vitendo hivi viovu vya wapagani na akawaagiza kwamba badala ya kuchukua majina ya mungu zao wa uwongo, wanapaswa kutaja jina la Allah Ta\u2019ala wanapoanza kazi yoyote au kuanza mradi wowote.<\/p>\n<p>Kwa hakika, maisha ya Muumini yanatawaliwa na imani na yakini kwamba ni kwa neema ya Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) tu na usaidizi wa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) ndipo matendo yote yanatimizwa. Kwa hivyo, Muumini anafundishwa kusoma Bismillah wakati wa kufungua au kufunga mlango, wakati wa kufunika chombo chochote, wakati wa kula au kunywa, wakati wa kuanza safari, wakati wa kupanda au kushuka kwenye usafiri, nk.<\/p>\n<p>Tunaposema &#8220;Bismillah&#8221; &#8211; kwa jina la Allah, kwa hakika tunasema kwamba tunaianza kazi yetu kwa jina la Allah Ta&#8217;ala na kwa usaidizi na baraka Zake tukufu. Kwa maneno mengine, tunakubali kwamba bila Allah Ta\u2018ala, hatuwezi kufanya kazi yoyote wala kukamilisha kazi yoyote, hata iwe kazi ndogo kiasi gani.<\/p>\n<p>Kimsingi, kila kipengele cha maisha ya Muumini kinapaswa kuanza kwa kuchukua jina la Allah Ta\u2019ala. Hivyo basi, kabla ya kuanza kusoma Qur&#8217;an Takatifu, tumeamrishwa kusoma Bismillah. Sababu ya kusoma Bismillah ni kutaka msaada na baraka za Allah Ta\u2018ala ili uweze kuisoma Qur&#8217;an Takatifu kwa usahihi na pia kuweza kuufahamu ujumbe wa Qur&#8217;an Takatifu na kupata mwongozo maalum kupitia kitabu cha Allah Ta&#8217;ala.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-3\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240505-WA0001.mp3?_=3\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240505-WA0001.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240505-WA0001.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Kumhimidi Allah Ta&#8217;ala<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\"><span id=\"1-2\" class=\"aya\">\u0627\u0644\u0652\u062d\u064e\u0645\u0652\u062f\u064f \u0644\u0650\u0644\u0651\u064e\u0647\u0650 \u0631\u064e\u0628\u0651\u0650 \u0627\u0644\u0652\u0639\u064e\u0627\u0644\u064e\u0645\u0650\u064a\u0646\u064e\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0662\ufd3e<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala)<\/em><\/p>\n<p>Sura hii inaanza na maneno \u00a0<span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u201c\u0627\u0644\u062d\u0645\u062f \u0644\u0644\u0647\u201d<\/span> (Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu subhaanahu wata&#8217;aala), kuashiria kwamba sifa zote kimsingi ni za Allah Ta\u2019ala pekee. Mtu ambaye anakisifu kitu chochote kilichoumbwa popote pale duniani hatimaye anamsifu Muumba wa vitu vyote &#8211; Allah Ta&#8217;ala, kwa sababu kusifiwa na kitu chochote ni kwa hakika kumsifu mtengenezaji wake.<\/p>\n<p>Kwa hiyo, Allah Ta&#8217;ala anapokuwa ndiye aliyeumba kila kitu, basi kukisifu kitu hicho ni kumsifu Allah Ta&#8217;ala, kwa sababu Yeye ndiye aliyekipa uzuri na fahari.<\/p>\n<p>Wakati mtu anapouchunguza ulimwengu na viumbe vilivyoumbwa ndani ya ulimwengu, basi kila kitu huvuta mazingatio ya mwanadamu kuelekea uzuri wake, lakini wakati mtu anapotazama nje ya pazia ili kuona ni nani anayedhibiti kila kitu katika ulimwengu na kuruhusu kufanya kazi kwa maelewano, utafahamu kuwa kwa hakika si mwingine ila ni Allah Ta\u2019ala peke yake.<\/p>\n<p>Kimsingi, kila kiumbe, katika fahari na uzuri wake, ni dhihirisho la utukufu wa Allah Ta\u2018ala peke yake.<\/p>\n<p>Mara tu mwanadamu ametambua kwamba kuna mmoja tu katika ulimwengu mzima ambaye anastahiki sifa zote, basi anapaswa kuelewa kwamba huyo pekee ndiye anafaa kuabudiwa. Kwa hivyo, tunaona kwamba ingawa maneno <span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u201c\u0627\u0644\u062d\u0645\u062f \u0644\u0644\u0647\u201d<\/span> (Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu subhaanahu wata&#8217;aala) imetumika kuashiria sifa, lakini, kwa maana inakata mzizi wote wa shirki (ushirikina) na ibada kwa viumbe vyote, na wakati huo huo, inasimamisha imani ya tawhid (kuleta imani katika Umoja wa Allah Ta\u2019ala).<\/p>\n<p>Kwa hivyo, tunaelewa kwamba aya ya kwanza kabisa ya Qur-aan Tukufu inaweka kanuni ya msingi ya Uislamu (yaani Tawhid \u2013 Umoja wa Allah Ta\u2018ala).<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-4\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240511-WA0002.mp3?_=4\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240511-WA0002.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240511-WA0002.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Mola Wa Ulimwengu Wote<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\"><span id=\"1-2\" class=\"aya\">\u0631\u064e\u0628\u0651\u0650 \u0627\u0644\u0652\u0639\u064e\u0627\u0644\u064e\u0645\u0650\u064a\u0646\u064e<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Mola wa Ulimwengu<\/em><\/p>\n<p>Neno \u201cRabb\u201d linamrejelea Kiumbe anayeleta uhayi kwa kila kiumbe , na kisha kuipa afya na kuipitisha hatua kwa hatua viwango tofauti vya maendeleo, mpaka kifikie ukamilifu. Kwa hivyo, tunaelewa kwamba sifa hii ya Rabb ni makhsusi kwa utakatifu wa Allah Ta\u2019ala na hakuna mtu mwingine yoyote anayeshiriki nayo.<\/p>\n<p>(ulimwengu) <span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u201c\u0639\u0670\u0644\u0645\u064a\u0646\u201d<\/span> inahusu ulimwengu tofauti au sayari tofauti ambazo Allah Ta\u2018ala ameziumba. Ulimwengu mmoja ni ulimwengu ambao tunaishi kwa sasa. Ulimwengu huu unaonekana kwa mwanadamu. Lakini, kuna ulimwengu au sayari zingine nyingi ambazo zimeumbwa na Allah Ta\u2018ala ambazo hazionekani kwa mwanadamu.<\/p>\n<p>Neno <span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">&#8220;\u0639\u0670\u0644\u0645\u064a\u0646&#8221;<\/span> pia linaweza kurejelea aina mbalimbali za viumbe kama vile ufalme wa binadamu, ufalme wa wanyama, ufalme wa majini na ufalme wa Malaa&#8217;ikah, nk. Viumbe hawa wakati fulani huitwa ulimwengu tofauti (ulimwengu wa mwanadamu, ulimwengu wa majini, ulimwengu wa wanyama, nk).<\/p>\n<p>Hivyo basi, Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) anaposema <span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u201c\u0627\u0644\u062d\u0645\u062f \u0644\u0644\u0647 \u0631\u0628 \u0627\u0644\u0639\u0670\u0644\u0645\u064a\u0646\u201d<\/span> (Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa ulimwengu wote), ina maana kwamba sifa njema zote ni za yule ambaye amevipa uhai kila kiumbe, anazipa afya na kuzikuza na kuwatunza tangu mwanzo hadi mwisho katika ulimwengu wanaoishi.<\/p>\n<p><strong>Mwingi wa Rehma na Mwenye kurehemu<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u00a0<span id=\"1-3\" class=\"aya\">\u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0652\u0645\u064e\u0670\u0646\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0650\u064a\u0645\u0650\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0663\ufd3e<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu<\/em><\/p>\n<p>\u201cAr-Rahmaan\u201d na \u201cAr-Rahim\u201d zote ni sifa za Allah Ta\u2019ala, zinazoashiria rehma yake iliyokithiri. Lakini, tofauti kati ya sifa hizo mbili ni kwamba \u201cAr-Rahmaan\u201d inaonyesha upana wa rehma Yake, wakati \u201cAr-Rahim\u201d inaonyesha undani wa rehma Yake.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-5\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240518-WA0006.mp3?_=5\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240518-WA0006.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/05\/AUD-20240518-WA0006.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Mfalme wa Siku ya Kuhukumu<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u00a0<span id=\"1-4\" class=\"aya\">\u0645\u064e\u0627\u0644\u0650\u0643\u0650 \u064a\u064e\u0648\u0652\u0645\u0650 \u0627\u0644\u062f\u0651\u0650\u064a\u0646\u0650\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0664\ufd3e<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Mfalme wa Siku ya Kuhukumu<\/em><\/p>\n<p>Licha ya Allah Ta\u2018ala kuwa ndiye Mfalme na Mmiliki wa viumbe wote na kila kilichomo katika dunia hii kila wakati, Allah Ta\u2018ala amejieleza Mwenyewe katika Aya hii kuwa yeye ni Mfalme na Mmiliki wa Siku ya qiyama kwa umakhsusi.<\/p>\n<p>Maulamaa wanaeleza kuwa sababu ya hili ni kwamba katika dunia hii Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) amempa mwanadamu umiliki wa baadhi ya vitu katika dunia, na Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) amewapa watu fulani mamlaka na udhibiti wa kuwatawala watu na sehemu fulani za ardhi. Lakini, Siku ya Kuhukumu, umiliki na mamlaka wa kila mtu utakwisha na hakutakuwa na kiumbe wowote ambae atakuwa na udhibiti au mamlaka juu ya mtu yoyote au kitu chochote. Itakuwa ni hukumu ya Allah Ta\u2019ala tu itakayotamba kwa watu wote siku hiyo. Kwa hiyo, Allah Ta\u2019ala alijieleza Mwenyewe kuwa ni Mfalme wa Siku ya kuhukumu.<\/p>\n<p><strong>Asili ya Dunia Hii Ikilinganishwa na Akhera<\/strong><\/p>\n<p>Allah Ta\u2019ala ameiumba dunia kuwa ni sehemu ya kuchuma matendo, na Akhera ni sehemu ya kulipwa kwa amali zake.<\/p>\n<p>Iwapo mtu ataleta Imaan na akafanya matendo mema katika dunia hii, atalipwa Jannah kwa matendo mema aliyoyafanya hapa duniani. Kwa hivyo, ikiwa mtu hatoleta Imaan na akaishi maisha ya ukafiri na shirki hapa duniani, basi ataadhibiwa na Jahannum huko Akhera kwa kutomuamini Allah Ta\u2018ala na Dini ya Uislamu.<\/p>\n<p>Mtu anapochunguza asili ya ulimwengu huu, anagundua kwamba haki kamili haiwezi kutendeka, kwa sababu mali, uwezo na umaarufu vipo mikononi mwa watu wema na waovu pia. Kwa hiyo, kuna wakati fulani haki inatendeka kwa mwenye kosa, na wakati fulani, mwenye kosa, kwa sababu ya umaarufu wake, anaweza kuepuka sheria za haki. Matokeo yake ni kwamba wasio na kosa wanachukuliwa kama wahalifu, na wahalifu wanachukuliwa kuwa wasio na kosa. Kwa hiyo, Allah Ta\u2019ala ameiumba Akhera kama makazi ambayo haki kamili itafikiwa kwa wote.<\/p>\n<p>Huo ndio uadilifu wa Allah Ta\u2019ala siku ya kiama kwamba lau mnyama mwenye pembe angemdhulumu mnyama asiye na pembe duniani kwa kumkata na pembe zake, basi Allah Ta\u2019ala atawafufua wanyama wote hawa wawili ili walipizane kisasi kati yao.<\/p>\n<p>Kimsingi, Allah Ta\u2019ala ameiumba Akhera kuwa ni sehemu ambayo haki kamili itafikiwa kwa viumbe wake wote na viumbe vyote vitalipwa kwa matendo yao. Ni kwa ajili hiyo ndio maana Allah Ta\u2019ala akajiita Mwenyewe kuwa ndiye Mfalme wa Siku ya Kuhukumu, kwa sababu itakuwa ni uamuzi na hukumu Yake pekee ndiyo itakayokuwa juu ya wote.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-6\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/06\/AUD-20240525-WA0000.mp3?_=6\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/06\/AUD-20240525-WA0000.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/06\/AUD-20240525-WA0000.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Kumgeukia Allah Ta\u2019ala Peke yake Kuomuomba Msaada<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\"><span id=\"1-4\" class=\"aya\"><span class=\"ayaNumber\">\u200f<\/span><\/span>\u00a0<span id=\"1-5\" class=\"aya\">\u0625\u0650\u064a\u0651\u064e\u0627\u0643\u064e \u0646\u064e\u0639\u0652\u0628\u064f\u062f\u064f \u0648\u064e\u0625\u0650\u064a\u0651\u064e\u0627\u0643\u064e \u0646\u064e\u0633\u0652\u062a\u064e\u0639\u0650\u064a\u0646\u064f\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0665\ufd3e<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Wewe peke yako tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.<\/em><\/p>\n<p>Katika lugha ya Kiarabu, neno ibaadah (kuabudu) lina maana ya kuonyesha unyenyekevu wa hali ya juu kutokana na upendo na heshima kubwa kwa mtu. Mtazamo huo wa kuonyesha kunyenyekea kwa moyo wote, kwa upendo na heshima kubwa, hauwezi kudhihirisha kwa yoyote isipokuwa Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<p>Kwa hiyo, tunaposema, \u201cWewe peke yako tunakuabudu,\u201d basi kwa hakika, tunatangaza kwamba tumejisalimisha kikamilifu kwa utiifu na ibada yake, kwa hisia ya kina ya upendo na heshima, kwa sababu ukweli ni kwamba yeye ndiye Muumba na Mlinzi wetu.<\/p>\n<p>Tunaposema, \u201cWewe tu tunakuomba msaada,\u201d tunakubali kwamba ni kwa uamuzi wa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) tu na hukumu yake kwamba jambo lolote linaweza kuwepo, na hivyo Yeye peke yake ndiye Mwenye udhibiti kamili juu ya mambo yetu yote. Kwa hivyo, ikiwa tutafuata njia za kidunia, basi ni kwa sababu ya amri yake kwamba tunafanya hivyo, na hatutazingatia njia za kufikia lengo letu, bali tutaelewa kuwa ni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) tu njia inaweza kufunguliwa.<\/p>\n<p>Kwa hivyo, njia yoyote ambayo Allah Ta\u2019ala amekataza mtu kuasili, mtu aepuke kuchukua njia hio, kwa sababu hii itakuwa sawa na kumpinga Allah Ta\u2018ala na kuweka utegemezi wa mtu kwenye haramu k.m. kuchukua mikopo yenye riba kutoka benki ili kuongeza mali ya mtu au kuchukua inshurance ili kulinda mali yako.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-7\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/06\/AUD-20240602-WA0001.mp3?_=7\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/06\/AUD-20240602-WA0001.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/06\/AUD-20240602-WA0001.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Asili Aya Tatu Za Kwanza<\/strong><\/p>\n<p>Katika aya tatu zilizotangulia, mwanadamu anakubali kumtegemea Allah Ta\u2018ala kwa wakati ulio pita, kwa sasa na siku zijao.<\/p>\n<p>Katika aya ya kwanza, Allah Ta\u2019ala anaeleza kuwa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) ni Mola wa walimwengu. Allah Ta\u2019ala Anasema: \u201cSifa njema zote ni za Allaah, Mola wa walimwengu wote\u201d. Kutokana na aya hii, tunapata kujua kwamba Allah Ta\u2019ala peke yake ndiye aliyempa mwanadamu uwepo wake na Allah Ta\u2019ala pekee ndiye anayemruzuku, kumlisha na kumtunza katika kila hatua ya maisha. Hivyo basi, mwanadamu anatakiwa kutambua utegemezi wake kwa Allah Ta\u2019ala hapo kwa muda ulio pita.<\/p>\n<p>Katika aya ya pili, Allah Ta\u2019ala anaeleza sifa yake kubwa ya kuonyesha wema na huruma kwa viumbe vyake vyote. Allah Ta\u2019ala Anasema: \u201cMwingi wa Rehma, Mwenye kurehemu.\u201d\u00a0Kutokana na aya hii, tunakuja kujua kwamba kila wakati ndani maisha ya mwanadamu katika dunia hii, mwanadamu anamtegemea Allah Ta\u2018ala kwa ajili ya kuendelea kwake na kuendelea kuishi kwake. Kwa hivyo, mwanadamu anapaswa kutambua utegemezi wake kwa Allah Ta\u2018ala katika wakati huu wa sasa pia.<\/p>\n<p>Katika Aya ya tatu, Allah Ta\u2019ala anaeleza kwamba Yeye ndiye Mola Mlezi wa Siku ya Kuhukumu. Allah Ta\u2019ala Anasema: \u201cMola Mlezi wa Siku ya Kuhukumu.\u201d\u00a0Kutokana na aya hii, tunapata kujua kwamba huko Akhera, mwanadamu atamtegemea Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) kwa ajili ya wokovu wake. Hivyo basi, mwanadamu anatakiwa kutambua utegemezi wake kwa Allah Ta\u2019ala katika siku zijazo.<\/p>\n<p>Baada ya mwanadamu kuelewa na kukiri kwamba alikuwa akimtegemea Allah Ta\u2019ala tangu zamani, anaendelea kumtegemea Allah Ta\u2019ala kwa sasa, na atamtegemea Allah Ta\u2019ala katika siku zijazo, kisha matokeo ya utegemezi huu ni kwamba mwanadamu anapaswa kumwabudu yeye peke yake, atafute msaada na usaidizi kutoka Kwake peke yake kwa sababu hakuna mwingine anayeweza kumsaidia, kumnufaisha kwa njia yoyote isipokuwa Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<p>Aya hii pia inatufundisha kwamba kwa vile mwanadamu anapaswa kumuabudu Allah Ta\u2018ala peke yake na kutafuta msaada kutoka Kwake peke yake, basi sajdah, tawaaf au kuomba dua kwa yoyote asiyekuwa Allah Ta\u2019ala haijuzu. Bali, mapenzi, khofu na matumaini ya mtu kwa Allah Ta\u2019ala yanapaswa kuwa makubwa zaidi kuliko mapenzi ya mtu, hofu na matumaini kwa kiumbe au kitu kingine chochote. Hakuna kitu kinachopaswa kuwa muhimu zaidi kwa mwanadamu kuliko uaminifu wake na uhusiano na Allah Ta\u2018ala.<\/p>\n<p>Kwa kumuomba Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aala) msaada Wake, tunamuomba usaidizi Wake, iwe kuhusiana na jambo lolote la dunia au Akhera.<\/p>\n<p><strong>Siri ya Surah Faatihah<\/strong><\/p>\n<p>Maulamaa wa Tafsiir wanaeleza kwamba asili ya Quran yote inapatikana katika Surah Faatihah, na asili ya Surah Faatihah inapatikana katika aya hii <span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u201c\u0625\u064a\u0627\u0643 \u0646\u0639\u0628\u062f \u0648\u0625\u064a\u0627\u0643 \u0646\u0633\u062a<span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u0639<\/span>\u064a\u0646<\/span>\u201d (Wewe peke yako tunakuabudu na kutoka Kwako tu tunakuomba msaada).<\/p>\n<p>Tunapoichunguza aya hii, tunakuta kwamba ina sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ni, \u201cWewe peke yako tunakuabudu\u201d, na sehemu ya pili ni, \u201cna kutoka Kwako tu tunatafuta msaada\u201d.<\/p>\n<p>Sehemu ya kwanza ya aya hii ni tamko la mtu kuwa mbali na shirki na kutomshirikisha yoyote na Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<p>Sehemu ya pili ni tamko la mtu kuweka amana na kumtegemea Allah Ta\u2019ala pekee, na kutoweka amana na kutegemea viumbe vyote ili kumtimizia haja na matakwa yake.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-8\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/07\/AUD-20240713-WA0012.mp3?_=8\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/07\/AUD-20240713-WA0012.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/07\/AUD-20240713-WA0012.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Maelezo Ya Sehemu ya Kwanza (Wewe peke yako tunakuabudu)<\/strong><\/p>\n<p>Kama ilivyoelezwa mwanzo, neno ibaadah linamaanisha kuonyesha unyenyekevu wa hali ya juu na kunyenyekea kwa mtu fulani kutokana na kumpenda sana na kumheshimu. Kwa hakika, kiwango hiki cha utiifu hakiwezi kupitishwa kwa yoyote asiyekuwa Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<p>Kwa hivyo, ikiwa mtu atampa mtu yoyote aina hii ya utiifu usio na kiwango na akamtii kinyume na amri ya Allah Ta\u2019ala, basi hii itazingatiwa kuwa ni shirki.<\/p>\n<p>Kutokana na hili, tunaelewa kwamba shirki (kumshirikisha Allah Ta\u2019ala) sio tu katika ibada na haifanyiki tu kwa kuabudu mawe na chuma kama wafanyavyo washirikina, bali pia hufanyika kwa kumtii, kumwabudu au kumpenda mtu kwa kiwango iliyohifadhiwa kwa ajili ya AllahTa\u2019ala.<\/p>\n<p>Katika Qur-aan Majeed, Allah Ta\u2018ala anazungumza kuhusu Mayahudi na Wakristo, na vitendo vya shirki walivyokuwa wakishiriki kwa kuwatii na kuwaheshimu wasomi na wachungaji wao kinyume na maamrisho ya Allah Ta\u2018ala. Allah Ta\u2019ala Anasema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u0627\u062a\u064e\u0651\u062e\u064e\u0630\u064f\u0648\u0653\u0627\u06df \u0627\u064e\u062d\u0652\u0628\u064e\u0627\u0631\u064e\u0647\u064f\u0645\u0652 \u0648\u064e\u0631\u064f\u0647\u0652\u0628\u064e\u0627\u0646\u064e\u0647\u064f\u0645\u0652 \u0623\u064e\u0631\u0652\u0628\u064e\u0627\u0628\u064b\u0627 \u0645\u0650\u0651\u0646 \u062f\u064f\u0648\u0646\u0650 \u0627\u0644\u0644\u064e\u0651\u0647\u0650<\/p>\n<p style=\"text-align: center;\">Wamewafanya wanachuoni wao wa kidini na watawa wao kuwa ni Mungu bali na Allah Ta\u2018ala\u2026 (Sura Taubah aya 31).<\/p>\n<p>Adiy bin Haatim (Radhiya Allaahu \u2018anhu) alikuwa Sahaabi wa Rasulullah (Sallallahu &#8216;alaihi wasallam) ambaye alikuwa ni Mkristo kabla ya kusilimu. Siku moja alikuja kwa Mtume (Sallallahu &#8216;alaihi wasallam) na akamuuliza: \u201cEwe Rasulullah (sallallahu &#8216;alaihi wasallam) kwa nini Qur&#8217;an Tukufu inawalaani wakristo kwa kuwachukua wanachuoni wao wa kidini kama mungu, na hali hawakuwa na hatia ya kufanya shirki kwa kuwaabudu?\u201d<\/p>\n<p>Mtume (Ssallallahu &#8216;alaihi wasallam) naye akamuuliza, \u201cJe, ni kweli kwamba wanachuoni wao wa kidini walipotangaza baadhi ya mambo kuwa ni haramu, ingawa Allah Ta\u2019ala ameyatangaza kuwa ni halali, na wao wakatangaza mambo mengi kuwa ni halali na hali Allah Ta\u2019ala akazitangaza kuwa ni haramu, kisha wakawatii wanachuoni wao kinyume na amri ya Allah Ta\u2019ala?\u201d<\/p>\n<p>Adiy bin Haatim (Radhiya Allaahu \u2018anhu) alikiri kwamba hii ni kweli. Hapo, Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) akasema: \u201cHivi ndivyo walivyokuwa wakiwaabudu wanachuoni wao.\u201d<\/p>\n<p>Hii inathibitisha kwamba Allah Ta\u2019ala peke yake ndiye mwenye haki ya kusimamisha yale ambayo ni halali na haramu. Kwa hivyo, ikiwa mtu anaamini kwamba mtu fulani pia ana haki ya kutangaza halaal na haramu, basi mtu huyo ametenda shirki, kama vile amemshirikisha mtu mwingine kuwa ni mshirika wa Allah Ta&#8217;ala katika haki ya kutangaza halaal na haramu, na hivyo ni kama anamwabudu mtu huyo.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-9\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/07\/AUD-20240721-WA0000.mp3?_=9\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/07\/AUD-20240721-WA0000.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/07\/AUD-20240721-WA0000.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Kurejea Kwa Wanachuoni Wa Kiislamu Kupata Uwongozo<\/strong><\/p>\n<p>Hili lisieleweke vibaya, kwa namna yoyote ile, kumaanisha kwamba haijuzu kwa mtu kuwarejelea wanachuoni wa kidini katika mambo ya dini. Sababu ni kwamba katika Quran Majeed, Allah Ta\u2018ala amewaamrisha wale waliopungukiwa na elimu warejee kwa wenye elimu ili kupata uongozo wa Dini. Allah Ta\u2019ala Anasema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u0641\u064e\u0627\u0633\u0652\u0626\u064e\u0644\u064f\u0648\u0627 \u0623\u064e\u0647\u0652\u0644\u064e \u0627\u0644\u0630\u0651\u0650\u0643\u0652\u0631\u0650 \u0625\u0650\u0646 \u0643\u064f\u0646\u062a\u064f\u0645\u0652 \u0644\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0639\u0652\u0644\u064e\u0645\u064f\u0648\u0646\u064e <span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0664\u0663\ufd3e<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Waulizeni wenye elimu ikiwa nyinyi hamjui\u2026 (Surah Nahl: 43).<\/em><\/p>\n<p>Hata hivyo, wenye elimu wanapaswa kuwaongoza watu kwa amri za Allah Ta\u2019ala, na wasiwapoteze kwa kuipotosha Dini na kuwalingania kwenye utiifu wao wenyewe.<\/p>\n<p><strong>Mifano Tofauti Ya Shirki<\/strong><\/p>\n<p>Mfano mwingine unaoingia katika kundi la shirki (kumshirikisha Allah Ta\u2019ala) ni:<\/p>\n<p>(1) kumtolea sadaka asiyekuwa Allah Ta\u2018ala k.m. kuchinja mnyama kwa jina la mchamungu.<\/p>\n<p>(2) kumuomba yoyote asiyekuwa Allah Ta\u2019ala wakati wa haja au dhiki.<\/p>\n<p>(3)\u00a0Kurukuu au kumsujudia yoyote asiyekuwa Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<p>(4) kufanya tawaf kumzunguka mtu au kitu chochote badala ya Nyumba ya Allah Ta&#8217;ala &#8211; Kaaba Tukufu.<\/p>\n<p><strong>Ufafanuzi wa Sehemu ya Pili (Kutoka Kwako Pekee tunatafuta msaada)<\/strong><\/p>\n<p>Sehemu ya pili ya Aya hii ni tamko la mtu kuweka amana yake na kumtegemea Allah Ta\u2019ala pekee, na kutoweka amana na kuegemea kwa kiumbe yoyote katika kumtimizia haja na matakwa yake.<\/p>\n<p>Inapaswa kueleweka kuwa ulimwengu huu ni ulimwengu wa sababu na athari. Kwa kuwa ni ulimwengu wa sababu na athari, shari\u2019ah inamfundisha mtu kuchukua njia za halali ili kutimiza mahitaji yake. Kwa hivyo, wakati wa hitaji, mtu huchukua huduma za daktari, wakili, seremala, mjenzi, n.k. kutimiza haja ya mtu.<\/p>\n<p>Kwa hiyo, tunapoombwa kufanya dua \u201ckutoka Kwako peke yako tunaomba msaada\u201d, je, Aya hii inatuzuia kunufaika na huduma za watu?<\/p>\n<p>Jibu la swali hili ni kwamba Aya hii haituzuii sisi kunufaika na huduma za watu, bali maana ya Aya hii ni kwamba mtu asiamini kuwa kiumbe chochote kile, hata akiwa nabii au mtakatifu, awe hai au amefariki kuwa na uwezo wa kusimamia mambo ya kidunia na kutimiza mahitaji ya mtu kama kuamini kuwa mcha Mungu fulani anaweza kumbariki mtu kupata watoto, au yeye ndiye anayesimamia rizki n.k. Kujiunga na imani hiyo ni haramu kwa sababu ni kumshirikisha Allah Ta\u2018ala katika sifa zake za kuhuisha na kufisha, kutoa rizki n.k.<\/p>\n<p>Kwa kifupi wa mambo ni kwamba tunapochukua msaada kutoka kwa watu au kuajiri huduma zao, basi hatuamini kwamba wana uwezo wa kutimiza mahitaji yetu, bali tunaamini kwamba ni Allah Ta&#8217;ala pekee ndiye atakayetengeneza njia. ufanisi na kusababisha hitaji letu kutimizwa.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-10\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/08\/AUD-20240803-WA0015.mp3?_=10\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/08\/AUD-20240803-WA0015.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/08\/AUD-20240803-WA0015.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Kutafuta Muongozo Kutoka Kwa Allah Ta\u2019ala<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\"><span id=\"1-6\" class=\"aya\">\u0627\u0647\u0652\u062f\u0650\u0646\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0635\u0651\u0650\u0631\u064e\u0627\u0637\u064e \u0627\u0644\u0652\u0645\u064f\u0633\u0652\u062a\u064e\u0642\u0650\u064a\u0645\u064e\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0666\ufd3e\u200f<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Tuongoze kwenye njia iliyonyooka<\/em><\/p>\n<p>Katika aya hii, neno <span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u201c\u0627\u0647\u062f\u0646\u0627\u201d<\/span> limetajwa ambalo linatoka kwenye neno <span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u201c\u0647\u062f\u0627\u064a\u0629\u201d<\/span> linalomaanisha mwongozo. Kwa maneno mengine, tunamuomba Allah Ta\u2019ala atujaalie uwongofu wa Allah Ta\u2019ala na atuonyeshe njia iliyonyooka.<\/p>\n<p>Hidaayah (mwongozo) ina maana ya kumuongoza mtu kwenye matakwa yake kwa wema. Sababu ya sisi kuomba dua kwa Allah Ta\u2019ala ili atujaalie mwongozo wa njia iliyonyooka ni kwamba mafanikio katika ulimwengu zote mbili (duniani na akhera) hayawezi kupatikana bila mwongozo wa Mwenyezi Mungu.<\/p>\n<p><strong>Daraja Tatu Ya Mwongozo<\/strong><\/p>\n<p>Maulamaa wanaeleza kuwa kuna viwango vitatu vya mwongozo. Kiwango cha kwanza cha mwongozo ni cha jumla na kinajumuisha viumbe vyote vilivyopo katika ulimwengu. Kiwango hiki cha muongozo kimetolewa na Allah Ta\u2018ala kwa kila kiumbe, ambacho kupitia kwao kinaweza kuwepo, kuendelea na kutimiza kazi yake.<\/p>\n<p>Kiwango hiki cha muongozo kimetajwa katika aya ifuatayo ya Qur-aan Majeed:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u0642\u064e\u0627\u0644\u064e \u0631\u064e\u0628\u0651\u064f\u0646\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0651\u064e\u0630\u0650\u064a \u0623\u064e\u0639\u0652\u0637\u064e\u0649\u0670 \u0643\u064f\u0644\u0651\u064e \u0634\u064e\u064a\u0652\u0621\u064d \u062e\u064e\u0644\u0652\u0642\u064e\u0647\u064f \u062b\u064f\u0645\u0651\u064e \u0647\u064e\u062f\u064e\u0649\u0670\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0665\u0660\ufd3e<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Akasema (Nabii Musa) (kumwambia Fir\u2019aun) \u201cMola wetu ni yule ambaye amekipa kila kitu umbo lake kisha akakiongoza. (Surah Taha aya 50)<\/em><\/p>\n<p>Vile vile, katika Qur\u2019aan Takatifu, Allah Ta\u2018ala anataja nyuki wa asali ukiongozwa na Allah Ta\u2018ala kupata nekta kutoka kwenye mimea na kujenga mzinga wake kwenye sehemu za juu na milima. Mfano mwingine ni ndege ambao wanaongozwa na Allah Ta\u2018ala kujenga kiota ili kuwakinga watoto wao kutokana na baridi, na kuhamia kwenye hali ya joto katika miezi ya baridi.<\/p>\n<p>Watu wengi wanaiona hii kama tabia ya silika ya mnyama, lakini kwa hakika, ni Allah Ta\u2018ala ambaye anaongoza kila kiumbe kutimiza kazi yake.<\/p>\n<p><strong>Daraja La Pili Ya Mwongozo<\/strong><\/p>\n<p>Daraja la pili ya muongozo si ya jumla, bali ni makhsusi kwa uumbaji huo unaozingatiwa kuwa umebarikiwa na akili na fahamu. Uumbaji huu unahusu mwanadamu na majini.<\/p>\n<p>Aina hii ya pili ya muongozo inatumwa kwa mwanadamu na majini na Allah Ta\u2018ala kupitia Ambiyaa (\u2018alaihimus salaam) na vitabu na maandiko yaliyoteremshwa na Allah Ta\u2019ala. Hivyo basi, mwanadamu na majini wanawajibika kuwamini Ambiyaa (\u2018alaihimus salaam) na kufuata shari\u2019ah waliyoileta kwa mataifa yao. Allah Ta\u2019ala Anasema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u0648\u064e\u0645\u064e\u0627 \u062e\u064e\u0644\u064e\u0642\u0652\u062a\u064f \u0627\u0644\u0652\u062c\u0650\u0646\u0651\u064e \u0648\u064e\u0627\u0644\u0652\u0625\u0650\u0646\u0633\u064e \u0625\u0650\u0644\u0651\u064e\u0627 \u0644\u0650\u064a\u064e\u0639\u0652\u0628\u064f\u062f\u064f\u0648\u0646\u0650\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0665\u0666\ufd3e\u200f<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Sikuwaumba majini na mwanaadamu ila waniabudu Mimi. (Surah dhaariyaat aya. 56)<\/em><\/p>\n<p>Ama wanyama, ingawa wana daraja la ufahamu, lakini kwa vile kiwango cha ufahamu wao unaupungufu ukilinganisha na mwanadamu, Allah Ta\u2019ala hakuwajibisha kufuata shari\u2019ah.<\/p>\n<audio class=\"wp-audio-shortcode\" id=\"audio-2288-11\" preload=\"none\" style=\"width: 100%;\" controls=\"controls\"><source type=\"audio\/mpeg\" src=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/08\/AUD-20240818-WA0000.mp3?_=11\" \/><a href=\"https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/08\/AUD-20240818-WA0000.mp3\">https:\/\/sw.alislaam.com\/wp-content\/uploads\/2024\/08\/AUD-20240818-WA0000.mp3<\/a><\/audio>\n<p><strong>Daraja La Tatu Ya Mwongozo<\/strong><\/p>\n<p>Daraja la tatu ya mwongozo ni maalum zaidi ikilinganishwa na daraja la ya pili. Kiwango hiki cha uwongofu kimebarikiwa kwa waumini wa kweli wanaomcha Allah Ta\u2018ala na wanaishi maisha ya taqwa.<\/p>\n<p>Kama jinsi daraja ya kwanza ya uwongofu inakuja moja kwa moja kutoka kwa Allah Ta&#8217;ala kwenda kwa viumbe mbalimbali, hivyo ndivyo daraja hii ya tatu ya uongozi nayo inashuka moja kwa moja kutoka kwa Allah Ta&#8217;ala kwenda kwa baadhi ya watu binafsi, inashawishi moyo kuchukuwa njia iliyonyooka, tofauti na daraja la pili ya mwongozo ambayo inamtegemea mwanadamu kufanya juhudi kuifuata.<\/p>\n<p>Kimsingi, tofauti kati ya ngazi la pili na la tatu la muongozo ni kwamba ngazi ya pili ya muongozo inaweza kufanana na kumwelekeza mtu kwa maneno au vitendo kwenye njia ya uwongofu, baada ya hapo inamtegemea mtu kufanya ijtihada na kufuata mwongozo huo.\u00a0Ama kiwango cha tatu cha mwongozo, basi kinaweza kulinganishwa na kumshika mtu mkononi na kumpeleka kwenye njia ya uongofu.<\/p>\n<p>Hivyo basi, katika Aya hii, tunapomwomba Allah Ta\u2019ala atuongoze kwa kusema<span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\"> \u201c<\/span><span id=\"1-6\" class=\"aya\"><span class=\"\" style=\"font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 14pt;\">\u0627\u0647\u0652\u062f\u0650\u0646\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0635\u0651\u0650\u0631\u064e\u0627\u0637\u064e \u0627\u0644\u0652\u0645\u064f\u0633\u0652\u062a\u064e\u0642\u0650\u064a\u0645\u064e<\/span><\/span>\u201d (Utuongoze kwenye njia iliyonyooka), basi ni daraja hii ya uongofu ndio tunakuwa tunamuomba Allah Taala.<\/p>\n<p>Katika Qur\u2019aan Majeed, Allah Ta\u2018ala anaponasibisha uwongofu Kwake Mwenyewe na si mwingine, ni daraja hii ya tatu ya uwongofu ndiyo inayorejelewa. Wakati ami wa Mtume (Sallallahu &#8216;alaihi wasallam), Abu Taalib, alipofariki dunia kwa ukafiri, Rasulullah (Sallallahu &#8216;alaihi wasallam) alihuzunika juu ya hali yake.<\/p>\n<p>Katika tukio hilo, Allah Ta\u2019ala alimwambia Mtume (Sallallahu &#8216;alaihi wasallam) akisema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u0625\u0650\u0646\u0651\u064e\u0643\u064e \u0644\u064e\u0627 \u062a\u064e\u0647\u0652\u062f\u0650\u064a \u0645\u064e\u0646\u0652 \u0623\u064e\u062d\u0652\u0628\u064e\u0628\u0652\u062a\u064e \u0648\u064e\u0644\u064e\u0670\u0643\u0650\u0646\u0651\u064e \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u064e \u064a\u064e\u0647\u0652\u062f\u0650\u064a \u0645\u064e\u0646 \u064a\u064e\u0634\u064e\u0627\u0621\u064f<span class=\"sign\">\u00a0\u06da<\/span> \u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Hakika wewe humwongozi umpendaye, lakini Mwenyezi Mungu humuongoza Amtakaye (kwenye njia iliyonyooka). (Surah Qasas aya 56)<\/em><\/p>\n<p>Hata hivyo, katika baadhi ya aya za Qur\u2019aan Majeed, Allah Ta\u2018ala anaponasibisha hidaayah na uongofu kwa Manabiu (\u2018alaihimus salaam) au waja wema, basi ni daraja la pili ya uongofu inayorejelewa. Kwa mfano, Allah Ta\u2019ala anawasifu Maulamaa wa Banu Israa\u2019il akisema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u0648\u064e\u062c\u064e\u0639\u064e\u0644\u0652\u0646\u064e\u0627 \u0645\u0650\u0646\u0652\u0647\u064f\u0645\u0652 \u0623\u064e\u0626\u0650\u0645\u0651\u064e\u0629\u064b \u064a\u064e\u0647\u0652\u062f\u064f\u0648\u0646\u064e \u0628\u0650\u0623\u064e\u0645\u0652\u0631\u0650\u0646\u064e\u0627 \u0644\u064e\u0645\u0651\u064e\u0627 \u0635\u064e\u0628\u064e\u0631\u064f\u0648\u0627<span class=\"sign\">\u00a0\u06d6<\/span>\u00a0\u0648\u064e\u0643\u064e\u0627\u0646\u064f\u0648\u0627 \u0628\u0650\u0622\u064a\u064e\u0627\u062a\u0650\u0646\u064e\u0627 \u064a\u064f\u0648\u0642\u0650\u0646\u064f\u0648\u0646\u064e\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0662\u0664\ufd3e<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Na tukawafanya waongozi wanaowaongoza watu wao kwa amri yetu, walipojifunza subira (na kuwa na msimamo juu ya dini yao), na wakawa na yakini katika Aya zetu. (Surah Sajdah v. 24)<\/em><\/p>\n<p><strong>Kundi Maalum Ambalo Limefadhiliwa na Allah Ta\u2018ala<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\"><span id=\"1-7\" class=\"aya\">\u0635\u0650\u0631\u064e\u0627\u0637\u064e \u0627\u0644\u0651\u064e\u0630\u0650\u064a\u0646\u064e \u0623\u064e\u0646\u0652\u0639\u064e\u0645\u0652\u062a\u064e \u0639\u064e\u0644\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650\u0645\u0652<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Njia ya wale uliowafadhilisha (kwa fadhila yako maalum)<\/em><\/p>\n<p>Katika aya iliyotangulia, tumeamrishwa tumuombe Allah Ta\u2019ala ili atuongoze kwenye njia iliyonyooka. Katika aya hii, Allah Ta\u2019ala anatufafanulia ni njia ipi iliyonyooka ya Dini. Allah Ta\u2019ala Anasema: \u201cNjia ya wale uliowafadhilisha (kwa fadhila Yako). Kwa maneno mengine, njia iliyonyooka ya Dini ni njia iliyofuatwa na wale ambao wamependelewa na kuchaguliwa na Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<p>Katika aya nyingine ya Qur-aan Majeed, Allah Ta\u2019ala anataja makundi manne ya waja kuwa ni wale aliowafadhilisha kwa fadhila zake maalum. Allah Ta\u2019ala Anasema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u0648\u064e\u0645\u064e\u0646 \u064a\u064f\u0637\u0650\u0639\u0650 \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u064e \u0648\u064e\u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u0633\u064f\u0648\u0644\u064e \u0641\u064e\u0623\u064f\u0648\u0644\u064e\u0670\u0626\u0650\u0643\u064e \u0645\u064e\u0639\u064e \u0627\u0644\u0651\u064e\u0630\u0650\u064a\u0646\u064e \u0623\u064e\u0646\u0652\u0639\u064e\u0645\u064e \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u064f \u0639\u064e\u0644\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650\u0645 \u0645\u0651\u0650\u0646\u064e \u0627\u0644\u0646\u0651\u064e\u0628\u0650\u064a\u0651\u0650\u064a\u0646\u064e \u0648\u064e\u0627\u0644\u0635\u0651\u0650\u062f\u0651\u0650\u064a\u0642\u0650\u064a\u0646\u064e \u0648\u064e\u0627\u0644\u0634\u0651\u064f\u0647\u064e\u062f\u064e\u0627\u0621\u0650 \u0648\u064e\u0627\u0644\u0635\u0651\u064e\u0627\u0644\u0650\u062d\u0650\u064a\u0646\u064e<span class=\"sign\">\u00a0\u06da<\/span>\u00a0\u0648\u064e\u062d\u064e\u0633\u064f\u0646\u064e \u0623\u064f\u0648\u0644\u064e\u0670\u0626\u0650\u0643\u064e \u0631\u064e\u0641\u0650\u064a\u0642\u064b\u0627\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0666\u0669\ufd3e\u200f<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Mwenye kumtii Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;alah) na Mtume, basi (Akhera) watakuwa katika kundi la wale ambao Mwenyezi Mungu amewafadhilisha (kwa fadhila yake maalum) yaani. Mitume, Mawalii, mashahidi na waja wema. Hawa ni wazuri kiasi gani! (Sura Nisaa v.69)<\/em><\/p>\n<p>Kutokana na makundi yote haya manne ya waja waliochaguliwa, Mitume ndio wenye daraja kubwa zaidi, wakifuatiwa na sideeqeen. Siddeeqeen ni wale ambao wamepata ukamilifu wa kiroho katika Dini na hali ya ndani na nje ya maisha yao inabakia juu ya ukweli na uaminifu wa kudumu kwa Allah Ta\u2019ala. Wa tatu katika daraja ni mashahidi &#8211; wale waliojitolea maisha yao kwa ajili ya Dini, na wa nne katika daraja ni waja wema wa Allah Taala.<\/p>\n<p><strong>Mfumo Mtukufu wa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aalah)<\/strong><\/p>\n<p>Katika aya hii, Allah Ta\u2019ala ametuamrisha kuwafuata waja wake wema, kwani wao ndio wameifahamu njia iliyonyooka. Sababu ni kwamba waja hawa wema wamejifunza elimu ya Dini na kitabu cha Allah Ta&#8217;ala kutoka kwa masheikh wao, ambao nao waliipata kutoka kwa masheikh wao, mpaka mfumo huu wa kupata Dini ukawafikia maswahaabah (Radhiya Allaahu &#8216;anhum) ambao waliipata kutoka kwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam).<\/p>\n<p>Kwa hiyo, tunaelewa kwamba katika Dini, sisi tunahitaji Kitaabullah (Vitabu vya AllahTa\u2019ala) na Rijaalullah (waja waliofadhiliwa na Allah Ta\u2018ala). Ikibidi mtu asome historia, atagundua kwamba tangu zamani, umekuwa ni mfumo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu Allah Ta&#8217;ala kwamba aliteremsha Kitaabullah (Vitabu vya mbinguni) pamoja na Rijaalullah (Manabii (&#8216;alaihimus salaam) na wafuasi wao wema). Hakuna kipindi kilichoshuhudiwa katika historia ya wanadamu ambapo Allah Ta\u2018ala aliteremsha kitaab kwa umma bila ya kuwapelekea Nabii.<\/p>\n<p>Dhamira ya Manabii (\u2018alaihimus salaam) ilikuwa ni kueleza matumizi sahihi ya kitaab cha Allah Ta\u2018ala kwa watu na kuwaonyesha jinsi ya kuishi maisha yao kwa mujibu wa maagizo yake.<\/p>\n<p><strong>Wajibu Wa Ummah huu<\/strong><\/p>\n<p>Kwa vile hakuna Mtume wala Nabii wa kuja na Shari\u2019ah mpya baada ya kuja kwa Uislamu (kwa sababu Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) ni Mtume wa mwisho na muhuri wa Mitume wote), Allah Ta\u2019ala ameupa Ummah huu heshima maalum kwa kuufanya kila mtu ndani ya ummah huu kuwa mdhamini wa Dini hii.<\/p>\n<p>Siku ya Qiyaamah, kila mtu katika ummah wetu utaulizwa kama alikuwa ameilinda amana hii kubwa ya Dini kulingana na uwezo wake. Pamoja na heshima hii, Allah Ta\u2019ala amewafadhilisha Maulamaa wa Ummah huu kwa kuwafanya warithi na wasaidizi wa kweli wa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) katika kuhifadhi Dini yake na Sunnah zake za barakah.<\/p>\n<p>Imepokewa kuwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: 'Traditional Arabic'; font-size: 16pt;\">\u0627\u0644\u0639\u0644\u0645\u0627\u0621 \u0648\u0631\u062b\u0629 \u0627\u0644\u0623\u0646\u0628\u064a\u0627\u0621<\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Maulamaa ni warithi wa manabii. (Sahih Ibnu Hibbaan #88)<\/em><\/p>\n<p>Kwa hivyo, katika zama hizi, kama Maulamaa wa Ummah watasimamisha Dini ya Allah Ta&#8217;ala na kuhifadhi Sunnah yake Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) katika maana halisi ya neno hili, hakika watastahiki na cheo la \u201cwarithi na makamu wa kweli wa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam).\u201d<\/p>\n<p><strong>Tofauti Kati Ya Manabii (\u2018alaihimus salaam) Na Maulamaa<\/strong><\/p>\n<p>Kuhusu Manabii (\u2018alaihimus salaam), wao ni tabaka la kipekee la waja wa Allah Ta\u2018ala ambao hawana dhambi. Walipokea wahyi kutoka kwa Allah Ta\u2019ala na hawakumuasi Allah Ta\u2019ala hata kwa muda mfupi katika maisha yao yote. Walitekeleza kila amri ya Allah Ta\u2019ala kwa jinsi walivyoamrishwa. Siku zote kulikuwa na ulinganifu kamili ulioshuhudiwa baina ya kitabu cha Allah Ta\u2018ala na matendo ya Manabii (\u2018alaihimus salaam). Kimsingi, Manabii (\u2018alaihimus salaam) walikuwa ndio chemchemi za uongofu (hidaayah) duniani.<\/p>\n<p>Kuhusu Maulamaa, hawapati wahyi wa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;alah) wala hawana dhambi. Kwa hiyo, hawawezi kulinganishwa na Ambiyaa (\u2018alaihimus salaam). Bali watafuatwa kama tu matendo yao yanaendana na Shariah (Kitabu cha Allah Ta\u2019ala na Sunnah za Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam)). Katika hali ambapo kuna mgongano kati ya matendo yao na Shari\u2019ah, hawatafuatwa. Badala yake, Shari\u2019ah itapewa upendeleo kuliko wao.<\/p>\n<p>Hivyo basi, tunaelewa kwamba Maulamaa wa Ummah hawachukuliwi kama vyanzo asili vya uongofu (hidaayah), kama vile msimamo wa Ambiyaa (\u2018alaihimus salaam). Bali, watachukuliwa tu kama waongozo kama tu wanaendelea kufuata Kitabu cha Allah Ta\u2018ala na Sunnah Mubarah za Mtume (Sallallahu alaihi wasallam).<\/p>\n<p>Kinyume chake, ikiwa watatoa amri na maagizo ya Ummah yaliyo kinyume na Kitabu cha Allah Ta\u2018ala na Sunnah za Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam), hawatofuatwa na kusikilizwa.<\/p>\n<p><strong>Waliochaguliwa Na Allah Ta\u2019ala<\/strong><\/p>\n<p>Ni mfumo wa Allah Ta\u2018ala kwamba Dini itabidi isomwe na kutafutwa kwa wale ambao wamebarikiwa na Dini. Kwa hiyo mtu atalazimika kuwatafuta waliochaguliwa na Allah Ta\u2018ala kuwa wabebaji wa kweli wa Dini yake.<\/p>\n<p>Katika mchakato wa kupata Dini kutoka kwa watu ambao walichaguliwa na Allah Ta\u2018ala, haitotosha kwa mtu kusoma tu maneno ya Qur&#8217;an Majeed na Hadith. Badala yake, mtu atalazimika pia kujifunza jinsi ya kutekeleza matendo kutoka kwao kupitia njia ya Sunnah. Kwa kuwa hili haliwezekani bila ya kubaki katika kundi la waja wema, waliochaguliwa na Allah Ta\u2018ala kwa muda fulani, Allah Ta\u2018ala ametuamrisha ndani ya Qur&#8217;an Majeed daima kubaki pamoja na wachamungu. Allah Ta\u2019ala Anasema:<\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\">\u064a\u064e\u0627 \u0623\u064e\u064a\u0651\u064f\u0647\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0651\u064e\u0630\u0650\u064a\u0646\u064e \u0622\u0645\u064e\u0646\u064f\u0648\u0627 \u0627\u062a\u0651\u064e\u0642\u064f\u0648\u0627 \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u064e \u0648\u064e\u0643\u064f\u0648\u0646\u064f\u0648\u0627 \u0645\u064e\u0639\u064e \u0627\u0644\u0635\u0651\u064e\u0627\u062f\u0650\u0642\u0650\u064a\u0646\u064e\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0661\u0661\u0669\ufd3e<\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata&#8217;aalah) na baki pamoja na waja wakweli (yaani waja wema, wasemao kweli kwa kauli na vitendo). (Sura Tawbah aya ya 119)<\/em><\/p>\n<p>Vile vile, tunaona kwamba Maswahabah (Radhiya Allaahu &#8216;anhum), kwa kubakia katika kundi la baraka la Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) na kupata Dini kutoka katika moyo wake wa mubaarak, walipata jina tukufu la &#8216;Swahaabah&#8217; (maswahaba watukufu wa Mtume [Sallallahu alaihi wasallam]).<\/p>\n<p>Kwa kuuchunguza kwa makini na kuuchunguza isnaad ambao Deen imetufikia, mtu atatambua kwamba kama vile Dini ilivyowasilishwa kupitia maneno na vitendo, ndivyo pia ilipitishwa kutoka moyo hadi moyo. Maswahabah (Radhiya Allaahu &#8216;anhum) walipata Dini kutoka katika moyo wa baraka wa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam), na Taabi&#8217;een (rahimahumullah) katika moyo za maswahaabah (Radhiya Allaahu &#8216;anhum), na hii iliendelea kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine. mpaka Deen hatimaye imetufikia sisi leo.<\/p>\n<p><strong>Kwa nini Allah Ta\u2019ala Hakutuamrisha Kufuata Njia ya Qur&#8217;an na Hadith?<\/strong><\/p>\n<p>Swali muhimu linalojitokeza katika wakati huu ni: \u201cKwa nini Allah Ta\u2018ala hakutuamrisha kushika njia ya Qur&#8217;an Majeed au njia ya Hadith, ambapo hivi viwili ni vyanzo vya msingi vya uongofu katika Dini?<\/p>\n<p>Jibu la swali hili muhimu ni kwamba lau kila mtu angerejea moja kwa moja kwenye Qur&#8217;an Majeed na Hadith ya Mtume (sallallahu alaihi wasallam) na kujaribu kufikia hitimisho lake mwenyewe kwa kuzingatia akili yake mwenyewe, Dini haitahifadhiwa tena katika njia ya Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) alikuwa ametufikishia.<\/p>\n<p>Badala yake, ingekuwa ni mchanganyiko wa matendo ya ibada yaliyochanganywa na matakwa na matamanio ya binaadamu, hivyo kusababisha uharibifu wa Dini. Hivyo basi, kwa ajili ya kuilinda na kuihifadhi Dini mpaka siku ya Qiyaamah, Allah Ta&#8217;ala ameamrisha ipitishwe njia ya waja wake waliochaguliwa na walioongoka, kwa sababu wao ndio wameielewa Qur&#8217;an Majeed na Sunnah kwa usahihi.<\/p>\n<p><strong>Njia ya Mayahudi na Wakristo<\/strong><\/p>\n<p class=\"\" dir=\"RTL\" style=\"text-align: center; font-family: usmaan_taha; font-size: 16pt; line-height: 38px;\"><span id=\"1-7\" class=\"aya\">\u063a\u064e\u064a\u0652\u0631\u0650 \u0627\u0644\u0652\u0645\u064e\u063a\u0652\u0636\u064f\u0648\u0628\u0650 \u0639\u064e\u0644\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650\u0645\u0652 \u0648\u064e\u0644\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0636\u0651\u064e\u0627\u0644\u0651\u0650\u064a\u0646\u064e\u00a0<span class=\"ayaNumber\">\u200e\ufd3f\u0667\ufd3e<\/span><\/span><\/p>\n<p style=\"text-align: center;\"><em>sio njia ya waliokasirikiwa na njia ya waliopotea.<\/em><\/p>\n<p>Katika aya hii, Allah Ta\u2019ala anazidi kubainisha njia iliyonyooka kuwa si njia inayofuatwa na waliomkasirisha Allah Ta\u2019ala, na wala njia ya waliopotea.<\/p>\n<p>Katika baadhi ya hadith, imeandikwa kwamba Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) alitaja kwamba tabaka hizi mbili za watu zinawahusu Mayahudi na Wakristo.\u00a0(Sunan Tirmizi #2954)<\/p>\n<p>Maulamaa wanaeleza kwamba ingawa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alitaja kwamba tabaka hizi mbili zinawahusu Mayahudi na Wakristo, Aya hii haiko kwao kwa makusudio yake tu, bali ni makafiri wote wanaowaiga Mayahudi na Wakristo katika njia zao za ukafiri pia kujumuishwa katika aya hii.<\/p>\n<p>Kwa ujumla, kuna sababu mbili za mtu kutofuata njia ya mwongozo. Sababu ya kwanza ni pale mtu anapomiliki elimu ya ukweli, lakini anaipinga, na sababu ya pili ni pale mtu anaposhindwa kutafuta ukweli kutokana na mtu kwa makusudi anaiga njia ya upotofu.<\/p>\n<p>Kuhusu Mayahudi, basi walikuwa na elimu, lakini waliipinga kwa ukaidi na kukataa ukweli kwa makusudi wakachukuwa njia ya upotevu. Kwa hiyo, Allah Ta\u2019ala akawataja katika Aya hii kuwa ni \u201cwale waliokasirikiwa\u201d.<\/p>\n<p>Ama Wakristo, basi hawakuwa na elimu ya haki kama Mayahudi, wala hawakuwa na nia ya kupata ukweli. Kwa hivyo, kwa makusudi walichukuwa njia ya upotovu na wakafuata matamanio yao. Kwa hiyo, Allah Ta\u2019ala anawataja kuwa ni \u201cwale waliopotea\u201d.<\/p>\n<p>Kutokana na aya hii tunaelewa kuwa ili mtu aongoke sawa sawa kama inavyomlazimu mtu kutekeleza matendo mema na kutekeleza maamrisho ya sharia, basi hivyo ndivyo ni muhimu kwa mtu kujiepusha na kumuasi Allah Taala. kwa kutenda madhambi, na hivyo kuwaiga maadui wa Allah Ta\u2019ala.<\/p>\n<p><strong>Hadith-ul-Qudsi Kuhusu Surah Faatihah<\/strong><\/p>\n<p>Hadith-ul-Qudsi inataja kwamba aya tatu za mwanzo za Surah Faatihah ni katika kumsifu Allah Ta\u2018ala, wakati aya tatu za mwisho za Surah Faatihah ni dua kwa manufaa ya waja wake. Ama aya ya katikati ya Surah Faatihah (aya ya nne), basi Aya hii ina sifa zote mbili za Allah Ta\u2019ala na dua.<\/p>\n<p>Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) ametaja kuwa Allah Ta\u2019ala anasema:<\/p>\n<p>Nimeigawanya Sura Faatiha katika sehemu mbili kati Yangu na mja Wangu, na kwa mja wangu kitakuwa kile anachokiomba. Mja anaposoma Aya ya kwanza na kusema: \u201cSifa njema zote ni za Allah Ta\u2019ala, Mola wa walimwengu wote,\u201d basi Allah Ta\u2019ala husema: \u201cMja wangu amenisifu&#8221;.<\/p>\n<p>Wakati mja (anaposoma Aya ya pili na) anasema, \u201cMwingi wa Rehma, Mwenye kurehemu,\u201d Allah Ta\u2019ala husema, \u201cMja wangu ametukuza fadhila yangu.\u201d<\/p>\n<p>Wakati mja (anaposoma Aya ya tatu na) akisema, \u201cMola wa Siku ya Qiyaamah,\u201d basi Allah Ta\u2019ala husema, \u201cMja wangu amenitukuza.<\/p>\n<p>Mja anaposoma Aya ya nne na kusema: \u201cWewe peke yako tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada,\u201d basi Allah Ta\u2019ala husema, \u201cHii ni baina Yangu na mja Wangu (yaani. katika haya ni sifa zangu na dua kutoka kwake kwangu), na kwa mja wangu atapata anachokiomba.\u201d<\/p>\n<p>Wakati mja (anaposoma aya tatu za mwisho na) anasema: \u201cTuongoze kwenye njia iliyonyooka \u2013 njia ya wale uliowaneemesha (kwa neema Yako makhsusi), si njia ya waliokasirikiwa na wala si njia ya wale walio potea, basi Allah Ta\u2019ala anasema: \u201cHii ni kwa ajili ya mja wangu, na kwa mja Wangu litakuwa lile analoliomba (yaani nitampa muongozo wa njia iliyonyooka na nimwokoe asikanyage katika njia ya wale waliopata ghadhabu yangu na njia ya waliopotea).\u201d (Sahih Muslim #395)<\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>\u0628\u0650\u0633\u0652\u0645\u0650 \u0627\u0644\u0644\u0651\u064e\u0647\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0652\u0645\u064e\u0670\u0646\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0650\u064a\u0645\u0650\u00a0\u200e\ufd3f\u0661\ufd3e\u200f\u00a0\u0627\u0644\u0652\u062d\u064e\u0645\u0652\u062f\u064f \u0644\u0650\u0644\u0651\u064e\u0647\u0650 \u0631\u064e\u0628\u0651\u0650 \u0627\u0644\u0652\u0639\u064e\u0627\u0644\u064e\u0645\u0650\u064a\u0646\u064e\u00a0\u200e\ufd3f\u0662\ufd3e\u200f\u00a0\u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0652\u0645\u064e\u0670\u0646\u0650 \u0627\u0644\u0631\u0651\u064e\u062d\u0650\u064a\u0645\u0650\u00a0\u200e\ufd3f\u0663\ufd3e\u200f\u00a0\u0645\u064e\u0627\u0644\u0650\u0643\u0650 \u064a\u064e\u0648\u0652\u0645\u0650 \u0627\u0644\u062f\u0651\u0650\u064a\u0646\u0650\u00a0\u200e\ufd3f\u0664\ufd3e\u200f\u00a0\u0625\u0650\u064a\u0651\u064e\u0627\u0643\u064e \u0646\u064e\u0639\u0652\u0628\u064f\u062f\u064f \u0648\u064e\u0625\u0650\u064a\u0651\u064e\u0627\u0643\u064e \u0646\u064e\u0633\u0652\u062a\u064e\u0639\u0650\u064a\u0646\u064f\u00a0\u200e\ufd3f\u0665\ufd3e\u200f\u00a0\u0627\u0647\u0652\u062f\u0650\u0646\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0635\u0651\u0650\u0631\u064e\u0627\u0637\u064e \u0627\u0644\u0652\u0645\u064f\u0633\u0652\u062a\u064e\u0642\u0650\u064a\u0645\u064e\u00a0\u200e\ufd3f\u0666\ufd3e\u200f\u00a0\u0635\u0650\u0631\u064e\u0627\u0637\u064e \u0627\u0644\u0651\u064e\u0630\u0650\u064a\u0646\u064e \u0623\u064e\u0646\u0652\u0639\u064e\u0645\u0652\u062a\u064e \u0639\u064e\u0644\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650\u0645\u0652 \u063a\u064e\u064a\u0652\u0631\u0650 \u0627\u0644\u0652\u0645\u064e\u063a\u0652\u0636\u064f\u0648\u0628\u0650 \u0639\u064e\u0644\u064e\u064a\u0652\u0647\u0650\u0645\u0652 \u0648\u064e\u0644\u064e\u0627 \u0627\u0644\u0636\u0651\u064e\u0627\u0644\u0651\u0650\u064a\u0646\u064e\u00a0\u200e\ufd3f\u0667\ufd3e\u200f Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa ulimwengu wote. Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu. Mfalme wa Siku ya kuhukumu. Wewe peke yako tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada. Tuonyeshe njia &hellip;<\/p>\n","protected":false},"author":4,"featured_media":1019,"comment_status":"closed","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"footnotes":""},"categories":[22],"tags":[],"class_list":["post-2288","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","","category-tafseer"],"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/2288","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/users\/4"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcomments&post=2288"}],"version-history":[{"count":36,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/2288\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":2769,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/2288\/revisions\/2769"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/media\/1019"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fmedia&parent=2288"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcategories&post=2288"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/sw.alislaam.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Ftags&post=2288"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}